AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Aliyekuwa mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro, Said Meck Sadiki amesema uteuzi aliyoufanya Rais John Magufuli kwa kiongozi wa Chama cha ACT- Wazalendo, Anna Mghwira kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, ni sahihi.
Sadiki aliliambia gazeti la Habarileo, kuwa Rais hajakosea kumteua Mghwira kuwa kiongozi wa mkoa wa Kilimanjaro kwani mwana mama huyo ni mchapakazi, mzalendo na asiye na ubaguzi, na uongozi unahitaji mtu wa aina hiyo.
Meck alisema kuna maeneo matano ambayo angependa mteuliwa huyo ayape kipaumbele ikiwa ni pamoja na uharibifu wa mazingira na utunzaji wa vyanzo vya maji. Alisema kama mazingira yataharibiwa zaidi ndani ya miaka 10 mkoa utakuwa jangwa na kukumbwa na baa la njaa. Katika eneo hilo, alitaka Mghwira ashirikiane na taasisi na viongozi wengine kutunza mazingira na vyanzo vya maji.
Hata hivyo eneo jingine alisema ni uvushwaji wa bidhaa za magendo kutoka Tanzania kwenda Kenya. Alisema mkoa unakosa mapato mengi kutokana na mbinu za ujanja za wafanyabiashara wasio waaminifu. Alimtaka kama Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa kujipanga vyema kudhibiti hilo. Dawa za kulevya Alisema kuwa zimekuwa zikiathiri maendeleo ya mkoa.
Bi Anna anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Saidi Meck Sadiki.
Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.
Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA
Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK