Bajeti Kuu ya Serikali 2017/18..Pato la Mtanzania Laongezeka kwa Asilimia 11...!!!

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Pato la kila mtanzania kwa mwaka 2016 limeongezeka kwa asilimia 11 kutoka shillingi 1,918,897 kwa mwaka 2015 mpaka kufikia shilling 2,131,299 kwa mwaka 2016.

Takwimu hizi zimebainishwa na Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt Philip Mpango wakati akiwasilisha Bungeni Mjini Dodoma Taarifa ya Hali ya Uchumi ya mwaka 2016 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa mwaka 2017/2018.

Akifafanua kuhusu ongezeko hilo Mhe. Dkt Philip Mpango amesema kuwa Pato la Taifa kwa mwaka 2016 lilifikia Shillingi million 103,744,606 kwa bei za mwaka husika na kiasi hiki kiligawanywa kwa idadi ya watu 48,676,698 walipo Tanzania Bara na kufanya wastani wa Pato la kila mtanzania kufikia kiasi cha Shillingi 2,131,299.

Ameeleza kuwa kwa thamani ya Dola za Marekani, wastani wa pato la Kila mtu liliongezeka kutoka Dola 967.5 mwaka 2015 hadi Dola 979.1 kwa mwaka 2016 ikionesha kuwa Tanzania inaelekea kwenye kundi la Uchumi wa kati.

“Serikali inaendelea kutatua changamoto mbalimbali ili tuweze kufikia Uchumi wa Kati kwa kuongeza fursa mbalimbali za uzalishaji nchini,” alisistiza Mhe. Dkt Mpango.

Mhe. Dkt. Phili Mpango ameongeza kuwa Serikali imejipanga kuboresha shughuli za uzalishaji wa tija katika Sekta zinazoajiri hususan katika Sekta ya Kilimo cha mazao,Ufugaji na Uvuvi.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad