Jinsi Ya Kujiweka Wa Thamani Kwa Mpenzi Wako

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Marafiki zangu tunaendelea na mada yetu ambayo kwa hakika imekuwa ndefu lakini yenye manufaa makubwa kwenye uhusiano wetu. Nilianza kwa kueleza kwamba yapo mambo mengi sana ambayo husababisha thamani ya mtu kushuka kwa mpenzi wake.

Nilishazungumza mengi katika matoleo yaliyopita lakini leo nitaendelea na kukazia zaidi kwenye athari za kuharakisha faragha. Karibu darasani.

ATHARI ZA KUHARAKISHA FARAGHA
Wiki iliyopita nilifafanua zaidi matatizo ya moja kwa moja ambayo mtu anaweza kuyapata kwa kuharakisha faragha ambapo nilisema kwamba kuna suala la kuchokwa na kuonekana wa kawaida.

Lingine ni kuonekana mwepesi kwenye suala la mapenzi hivyo mwanaume kuwa na mashaka kwamba hata kama akifikia uamuzi wa kukuoa unaweza kuwa mwepesi kutoa penzi kwa wengine kama ulivyofanya kwake. Tuangalie vipengele vinavyofuata.

(i) Hupunguza thamani
Heshima ya penzi ni kwenye ndoa. Kuna uwezekano mkubwa sana wa kushushwa thamani baada ya kutoa penzi. Wanaume wengi huanza kuwa wasumbufu (kama ni kasumba yao) kwa wapenzi wao baada ya kutoka nao kimapenzi.

Pamoja na kwamba ni tendo la furaha lakini kwa mwanamke linampa unyonge na wakati mwingine huwa mwanzo wa utumwa wa mapenzi kwa kuogopwa kuachwa wakati tayari ameshatumika!
Hebu jiulize; utatumia/utatumika kwa wangapi? Ukifikiri kwa makini juu ya jibu la swali hili bila shaka utabadilisha mtazamo wako.

(ii) Hupunguza msisimko
Penzi la kienyeji mara nyingi hata wahusika huwa wanajua kabisa kuwa wanakosea. Makosa haya husababisha kupoteza msisimko wa ndani. Ni jambo la kisaikolojia sana na huenda muathirika asigundue tatizo hili kupitia dalili za kitaalamu atakazozionesha.

Mkishaibana huko nje huwa kuna uwezekano mkubwa zaidi wa kupoteza msisimko wa kawaida. Mfano mawasiliano hupungua, hamu ya kuonana inapungua sana n.k
Hapa nisipoteze muda sana, wengi mnafahamu inavyokuwa; MWANAUME AKISHATEMBEA NA MWANAMKE, TARATIBU ATAANZA KUJIWEKA PEMBENI. Kama alikuwa anapiga simu mara nne au tano kwa siku, hupunguza idadi na wakati mwingine hupitisha siku nzima kabisa.

Mbaya zaidi, unaweza kumpigia wewe na bado asipokee, ukituma ujumbe mfupi hatajibu au atachelewa. Kesi nyingi sana nilizokutana nazo za wanawake wanaolalamika wapenzi wao kubadilisha utaratibu wa mawasiliano, baada ya kuwahoji walisema jambo hilo limejitokeza baada ya kuwapa penzi.

MUHIMU KWAKO KUJUA
Mwanaume wa aina hii ni yule ambaye hakuwa na mpango wa ndoa baadaye au hakuwa na uhakika na aina ya uhusiano anaotaka kwa mwanamke wake.

Sasa jiulize, ikiwa alikuwa kwenye majaribio, utajaribiwa na wangapi? Tumia hekima rafiki yangu ili kujinasua katika mtego huu.

(iii) Upungufu
Ukishautoa mwili wako kwa mwanaume, kama ni aina ya wale ambao huchunguza sana ni rahisi kukutoa kasoro. Utamsikia akisema, aaah! Huyu mwanamke bwana ana sijui nini...hakuna hoja za maana.

Kikubwa unachotakiwa kuelewa hapa ni kwamba kuutoa mwili wako hovyo kunakupeleka kwenye kujichoresha na pengine kama umekutana na mwanaume kicheche ataishia kukutumia na kukuacha kama alivyokukuta!

(iv) Msimamo
Pamoja na kwamba wanaume wengi ndiyo hasa wanaokuwa wa kwanza kushawishi kupewa mapenzi, ukweli ni kwamba ni wepesi wa kulaumu (vipengele vilivyopita nilikazia zaidi) na kuwaona wenzi wao hawana msimamo na maisha yao.

Kukuweka kwenye kundi hilo kutakukosesha nafasi ya uhakika ya kuingia kwenye ndoa, maana wengi wanapenda kuwa na wenzi wenye msimamo thabiti.

(v) Mimba
Kuna suala la mimba. Nimekutana na kesi nyingi sana za aina hii. Wanaokutana kimwili na wenzi wao bila mpangilio huwa hawazingatii sana suala la mimba lakini inapotokea ndiyo huanza kuhangaika kutafuta ushauri.

(VI) Magonjwa
Kuharakia mapenzi kuna matatizo mengi. Ukiacha kuwa katika hatari ya kupata magonjwa ya zinaa pia kuna suala la ujauzito. Mathalan utakuta msichana amepata mimba isiyotarajiwa, anatafuta shotikati na kwenda kuitoa, hapo kuna matatizo mengine mengi anayoweza kuyapata kutokana na kitendo hicho.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad