Lowassa Aeleza Anachoamini ni Mwarobaini wa Wizi Kwenye Madini..!!!

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa ameeleza kile anachoamini kuwa ndio tiba halisi ya matatizo ya wizi katika sekta ya madini nchini. Amesema hayo siku chache baada ya Rais Magufuli kupokea ripoti ya pili ya mchanga wenye madini, uliokuwa ukisafirishwa kwenda nje ya nchi na kampuni ya Acacia.

Akizungumza na waandishi wa habari, Lowassa ambaye ni mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema, alisema kuwa ili matatizo ya unyonyaji kwenye sekta hiyo yakabiliwe kikamilifu, Tanzania inapaswa kuandika katiba mpya.

Alisema kuwa mapungufu katika mikataba na sheria ya madini yamekuwa yakilalamikiwa na wapinzani kwa miaka mingi ndani ya Bunge lakini maoni yao hayakukubalika.

“Wapinzani wameshasema sana, wakasema mikataba hii iletwe tuitazame upya kwenye Bunge, lakini walikataliwa,” alisema akiwataja baadhi ya makada wa vyama vya upinzani kama Tundu Lissu, John Mnyika na Zitto Kabwe waliowahi kuwasilisha ombi hilo.

“Walikataliwa kwa sababu siri yake, jambo hili haliko kwenye katiba. Ndio maana mimi nasema tiba yangu moja kubwa ni kuhakikisha tunapata katiba mpya. Katiba ambayo itazitangatia maslahi ya wananchi katika kugawanya rasilimali zake,” aliongeza.
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Duh! Watu wote waseme, hata wewe Lowasa pia???

    ReplyDelete

Top Post Ad