Nimeamua Nithubutu Ingawa Nina Mtaji Pungufu ya Laki Saba. Nawe Waweza Jaribu Mahali Unapoishi..!!!

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Tatizo kubwa kwa sisi wanavyuo hatuwazi nje ya box,kila mtu akipata vilaki kadhaa(mwanachuo) anakimbilia kufungua banda la chipsi.OK fine malengo yako baada ya hilo banda?.

Ok Mimi ni mwanachuo wa mwaka wa pili,nimeamua kuja na ubunifu tofauti wa biashara yangu.Nimendunduliza nikafikisha laki sita na nusu na ninadream zakuja kuwa bakharesa hapo baadae.Unajua nimefanya nini?.

Nimetafuta vijana waaminifu wawili niliosoma nao wakafeli school.Mmoja yupo huko hom(mkoani) mwingine nimemtumia nauli elfu 50 aje dsm nikae nae geto(kashafika).

Nimechofanya yule wa mkoani(ninamuamini sana) nilimtumia laki nne na nusu,akanunua mchele kg 400.kilo kwa sasa mchele mpya ni 1000Tzsh.Kwahiyo apo ilienda sh laki nne.akabakiwa na sh elfu arobain,nmejumlisha na hela yakutoa mchele mashineni na magunia yakuuwekea.

Baada ya hapo akaenda tafuta usafiri ambao kila kg 100,wamemtoza sh elfu 10000.kwahiyo kg 400 akawa kamaliza ela mpaka mzigo kufika dar.

Sasa unajua nmeamua kuifanya vipi hii biashara.Mimi nauza kuanzia Kg 5. Kwa shilling 1800 kila kilo.Nmechukua oda ya mama ntilie wanao uza chakula chuo nacho somea,pia na baadhi ya mama ntilie wamtaani.

Pia nawauzia wanafunzi wanaojipikia kwenye magheto.Jambo la msingi nimelofanya nikuwa mtu akihitaji mchele ananipigia simu nampelekea mchele mpaka mahali anapokaa.
Kama itakuwa mbali sana ambapo nitahitaji usafiri basi itabidi kg1 mteja ainunue kwa sh 1900.

Mchele ninaouza quality yake kwenye maduka ya mitaani ni sh 2200.
Sasa nimeanza na hizi kg 400,ambazo nikiziuza kwa kg1, sh 1800. Nitatoa sh 720000.Na hii nategemea ndani ya siku 10, mpaka 12 nitakuwa nimeshaipata, kwahiyo awamu ijayo nitatuma kg zaidi ya 580 kama bei haitopanda 

Tumekubaliana nahawa jamaa zangu wawili tutaanza kulipana japo hela ya sabuni baada ya miezi minne.Na huku nikiwa nimesubiri hela ya bum nitoe kama laki tatu niongezee ili mtaji ukue baada ya mauzo.

Pia nimekopa mizani nitakuwa nalipa kidogo kidogo kadiri mauzo yangu yatakavyokuwa.

Chakula ambacho nakula mie na huyu jamaa yangu kipo nje ya bajeti ya mtaji.

Na wewe mwanafunzi mahali ulipo/mtu mwenye mtaji mdogo waweza jaribu hii nahakika itakulipa.

Au kama mtu yeyote mwenye ushauri zaidi namna nitakavyoboresha zaidi anaweza kunisaidia(tusaidia).

Sitaki kazi.
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad