Simba Sc Yasajili Wawili Kutoka Mwanza..Kaburu Adai Anamajina Mengine Sita Makubwa Yatasaini Simba Hivi Karibuni..!!

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Klabu ya Simba SC imeanza kuimarisha kikosi chake kuelekea msimu ujao wa Kombe la Shirikisho la Afrika, baada ya jana kukamilisha usajili wa walinzi wawili kutoka jijini Mwanza.

Simba imevuta beki wa kushoto, Jamal Mwambeleko kutoka Mbao FC na beki wa kati Yussuf Mlipili kutoka Toto Africans ambao wote wametokea jijini Mwanza

Kwa mujibu wa Makamu wa Rais wa Simba SC, Geoffrey Nyange ‘Kaburu’ amesema kwamba, Mlipili amesaini miaka mitatu na Mwambeleko amesaini miaka miwili adai mchezaji Mlipili anatua kwa mara ya kwanza kabisa Simba SC, wakati Mwambeleko yeye ni kama anarudi nyumbani sababu amewahi kuchezea timu ya vijana ya Wekundu hao wa Msimbazi.

Mbali na hilo Kaburu baada ya kukamilisha usajili huo amesema mashabiki na wapenzi wa Simba wakae mkao wa kula kwa taarifa za kuvutia zaidi kuhusu usajili wa timu yao hiyo ambao unaendelea sasa.

“Kwa ujumla nina wachezaji sita ambao wamekwishakamilisha usajili wao hapa Simba, lakini nitakuwa nachomoa mmoja mmoja namtambulisha” Alijinasibu Kaburu 

Mlipili na Mwambeleko wote waliichezea Simba SC kwa mara ya kwanza kwenye mashindano ya SportsPesa Super Cup 2017 huku Simba ikitolewa kwa penalti 5-4 na Nakuru All Stars ya Kenya.
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad