MBOWE Usipobadili Aina ya Siasa CHADEMA Hakika Tutakudai na 2020 Mtaangukia PUA Tena....

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Naomba juu ya hili nitumie nafasi hii kimshauri kamanda wangu kubadili aina ya siasa anayotaka kwenda na utawala wa awamu hii. Sina mashaka kabisa na ufundi wa siasa kwenye kichwa cha Kamanda Mbowe lakini naona kama kuna mtu anamshauri sivyo.

Nisiwe mnafki na uzi huu usiwe chanzo wa kufungua midomo ya maadui wakubwa wa CHADEMA wasiompenda Mbowe na wanachema kwa ujumla.Ni kazi nzuri sana anayofanya Mh Mbowe lakini muda unakimbia, CCM wameamua kutumia mikutano yao kujinadi kwa koti la ziara za Serikali.Hii siao sawa.


Kwa bahati mbaya sana niko nje ya nchi kwa kuda kidogo kunoa ubongo na ningekua nyumbani pasinashaka ningeufikisha ujumbe huu kwa mdogo moja kwa moja, naomba nieleweke hivyo.Ningemweleza Mh Mbowe kila kitu na namna ya kukabiliana na CCM.


CHADEMA kuna front lines nzuri sana za vijana haraka wa kazi walioiva kisiasa mfano kina Halima Mdee,Lundu Lissu,Boniface Jacob,John Mnyika Heche ,Kigaila,Waitara ,Salum Mwalimu,Sugu,Bint Peneza,Godbless Lemma,Davidi Kafulila, Petter Lijualikali na makamanda wengineo. Hawa wakipewa mwelekeo mzuri ni watu wasioogopa kusonga mbele.Hawa ni vijana jasiri sana wanao uwezo wa kubadili taswira ya Chama nchi nzima mwezi mmoja tuu.Operation ya kukieneza chama inaweza kubuniwa vizuri kwa kuangalia mazingira,wakati na aina ya utawala tulip nao.Je,hili Mbowe analifikiria?


Tafadhali sana Mbowe, umma wa watanzania hauitegemei CCM kuwasemea matatizo yao zaidi ya Upinzani. Usipooze hivyo my brother, msijipe moyo kwa kusema mko vizuri ilihali kugikia 2020 ni kesho tu.


Najua watu watauliza kua siasa hizi zitafanikiwa vipi ikiwa mikutano imezuiliwa? Tutambue kua kufanya mikutano ya siasa ni utaratibu wa katiba ya nchi na sio maelekezo ya mtu binafsi,hatujazoea kuishi bila kufuata sheria. Sheria iko wazi, kinachwafanya kulalamikia nyoyoni ni kitu gani? Kwani mkifanya mikutano kwa kufuata taratibu za kisheri mtazuiliwa kwa sababu zipi ikiwa wao CCM wanafanya?


Ustaarabu mnaotaka kuuonesha kuepusha siasa za malumbano Mh Mbowe usitegemee kama mtaupata ustaarabu kutoka CCM, hawana utani wanatazama weakness zenu. Mkipigwa mkwara nanyi mnakaa kimya ndivyo mnavyojimaliza wenyewe.

Hebu mniambie nijue kitu kimoja, kama Pole pole anazunguka na kufanya mikutano ya hadhara maeneo mbali mbali ya nchi...Je, akitoka Benson Kigaila au Tumain Makene nae akaifanya hivyo kwani iwe kosa? CCM sio chama? CHADEMA sio chama?
Woga wako Mh Mbowe usiwaambukize hawa vijana wapambana. Wagawie majukumu wewe ukiwa msimamizi mkuu kazi oende. Siasa za kukaa kimya unabaki kilalamikia chini so siasa hizo.

By Mahanju/JF
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. hahahah! Unawachochea wenzako wanyee debe, wakati wewe upo ughaibuni!! Njoo huku TZ ndio uyasema na uongoze kuyatenda hayo usemayo........wakati huu sio ule, ukileta FYOKO una FYOKOLEWA...shabash

    ReplyDelete

Top Post Ad