Ni Marufuku Matangazo Kwenye Miito ya Simu- TCRA

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), imepiga marufuku matangazo ya biashara yanayowekwa mtumiaji anapopiga simu ili kutoa fursa kwa watumiaji kupata mawasiliano bila usumbufu.

Mkurugenzi wa TCRA, Mhandisi James Kilaba amesema jana (Ijumaa) kuwa mamlaka hiyo imepokea malalamiko mengi kutoka kwa watumiaji wa simu wakilalamikia matangazo hayo yanayotolewa na kampuni za simu.

Amesema tayari TCRA imeshaziandikia barua kampuni zote za simu kusitisha matangazo hayo na itakutana nazo kwa majadiliano ya kina Julai 6.

Amesema mamlaka haitambui utaratibu huo na inauchukulia kama kero kwa watumiaji wa simu ambao hutegemea kutumia njia hiyo ya mawasiliano kurahisisha mambo.

“Tuna imani mtu anapopiga simu ana shida ya haraka na anahitaji afanye mawasiliano, unapomuwekea matangazo kwa dakika tatu au nne ni usumbufu,” amesema.

Katika siku za karibuni imekuwa ni kawaida kwa mtu anayepiga simu kusikiliza wimbo au matangazo ya biashara na baadaye kuambiwa namba anayopiga haipatikani.
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad