R Kelly Yamkuta Makubwa 'Atuhumiwa Kwa Kuwanyanyasa Kingono Wanawake

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Mwanamuziki wa mtindo wa R&B R Kelly amekana madai kwamba anawazuia wanawake kadhaa katika dhehebu lake analotumia kuwanyanyasa.

Wakili wa mwanamuziki huyo alisema kuwa atatumia kila njia kuhakikisha kuwa wale wanaomtuhumu anawakabili kisheria ili kusafisha jina lake.

Ripoti ya BUzzFeed imemtuhumu mwanamuziki huyo kwa kuwabadili kimawazo wanawake walio karibu naye kwa lengo la kuimarisha usanii wao wa muziki.

Kelly tayari amewahi kukabiliwa na tuhuma za dhulma za kingono lakini hakupatikana na hatia.
Amekana kufanya makosa yoyote.

Ripoti hiyo iliowanukuu wazazi watatu inasema kuwa hawajawasiliana na wanao kwa miezi kadhaa ,na kwamba wanawake hao wote wakiwa na umri wa zaidi ya miaka 18 walikuwa wakidhibitiwa na msanii huyo.

Udhibiti huo unashirikisha chakula wanachokula na nguo wanazovaa ,wakati gani wa kuoga na kulala mbali na kufanya tendo la ngono yote hayo yakirekodiwa na msanii huyo.

Wanachama watatu walio karibu na mwanamuziki huyo pia walihojiwa na kusema kuwa wanawake sita wanaishi katika nyumba zinazosimamiwa na msanii huyo.

Iwapo watavunja sheria, wanasema wanawake hao huadhibiwa kwa kupigwa mbali na kutukanwa na msanii huyo kulingana na ripoti hiyo.

Baadhi ya wazazi wao wameripoti wasiwasi kwa polisi, lakini wanawake hao wanasema kuwa wamekubali kuishi katika nyumba hizo.

Wakili wa msanii huyo Linda Mesch alisema: Robert Kelly ameshangazwa na kukerwa kuhusu madai hayo mapya anayodai kutekeleza.
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad