SALAMU za Rais wa TFF, Jamal Malinzi Kutoka Gerezani Hizi Hapa

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Rais wa TFF anayemaliza muda wake Jamal Malinzi amewatumia salamu viongozi wa TFF na kuwatakia uchaguzi mwema unaotarajiwa kufanyika mwezi Agosti mwaka huu.

Aidha, Malinzi katika salamu hizo, ameishukuru Serikali ya awamu ya tano chini ya Rais Dk. John Pombe Joseph Magufuli, wadhamini mbalimbali, washirika na wadau wa soka kwa ushirikiano walioutoa katika kipindi chote cha uongozi wake.

Salamu hizo ambazo zimetolewa kupitiwa kwa mawakili wake zilieleza kuwa anaamini kwamba TFF watafanya uchaguzi vizuri na viongozi watakaopatikana wataweza kuendeleza programu muhimu.
Malinzi alilazimika kujiondoa kwenye uongozi wa TFF na kushindwa kutetea nafasi yake baada ya kuwekwa rumande tangu Juni 29 kwa tuhuma za ubadhirifu na matumizi mabaya ya madaraka.

Malinzi, Katibu wake, Selestine Mwesigwa pamoja na Mhasibu wa TFF, Nsiande Isawafo Mwanga walipelekwa rumande Juni 29 baada ya kusomewa mashitaka 28 ya kughushi na kutakatisha fedha kupitia akaunti ya TFF iliyopo katika banki ya Stanbic, Dar es Salaam.
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad