VIDEO Tundu Akigoma Kutoka Mahakani......

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

July 19, 2017 Mbunge wa Singida mashariki Tundu Lissu aligoma kutoka katika chumba cha Mahakama ya wilaya Dodoma alipokuwa akifanya shughuli zake za uwakili kwa kuhofia kukamatwa na Polisi waliosemekana kumsubiri nje wamkamate kwa tuhuma za uchochezi.

Akiwa ndani ya Mahakama, Tundu Lissu aliongea mbele ya Waandishi wa habari Dodoma na kusema kuwa alibaini njama za Polisi kutaka kumkamata baada ya kupata taarifa kutoka kwa Mke wake  na kwamba Polisi walianzia kumtafuta nyumbani Dar es salaam kabla ya kufahamu kuwa yuko Dodoma.

Kwenye hii video hapa chini Tundu Lissu anaonekana akielezea mkasa huo…
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

2 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. . Kwa bahati mbaya watu wa aina ya Tundu Lisu walitumika au kutumiwa bila ya wao wenyewe kujua kama wanatumika na mataifa ya kigeni hasa ya kibepari ili kuwapinga viongozi ambao wangeliletea Africa mafanikio makubwa ya kimaendeleo. Kwa bahati mbaya kuna baadhi ya viongozi wa Africa waliozamiria kuzikumboa nchi zao juu ya utegemezi wa mataifa ya magharibi walipoteza maisha yao katika mazingira ya kutatanisha aidha kwa kuuwawa kikatili au kupata magonjwa ya kutatanisha. Maadui wasioitakia mema Africa na kutaja demokrasia kama haki za watu lakini kwa upande wa nyuma waliwatumia akina Tundu Lisu kuliangamiza bara la Africa. Kama kweli ni demokrasia basi Egypt au Misri ulifanyika uchaguzi halali na raisi akapatikana halali kabisa bila ya doa lakini kwa kuwa hakuwa raisi anaehitajika na mataifa mabepari raisi huyo akapinduliwa mchana kweupe kabisa na kusekwa gerezani mpaka hivi sasa tunavyozungumza. Hakuna umoja wa mataifa au watu wa haki za binaadamu au mataifa mabingwa wa kulinda demokrasia duniani waliopigia kelele kilichotokea Egypt. Na hayo mataifa makubwa yanayojiita mabingwa wa demokrasia duniani wamekuwa ndio mataifa kipenzi wa raisi wa sasa Egypt ambae hapana shaka hata kidogo yakwamba ni dikteta halisi. Sasa unashangaa sana unapoona watu wanaojiita wasomi kama Tundu Lisu na hata rafiki yake Zitto Kabwe wanapohangaika kuyalimisha mataifa hayo ya kibepari kumuazibu Magufuli na Tanzania yake kisa Uchungu na juhudi anazochukuwa Magufuli kuhakikisha Tanzania inaondokana na umasikini. Kisa jitihada za makusudi za muheshimiwa Magufuli za kuwahamasisha watanzania kufanya kazi kwa bidii baada ya kukaa vibarazani na kuhangaika na mikutano ya kisiasa na kusikiliza ahadi hewa. Hata siku ya hukumu siku ya mwisho ya hesabu mbele ya Mungu Muweza wa kila kitu hakuna kitachosema isipokuwa mizani katika matendo ya mtu. Na Mizani ya muheshimiwa Magufuli mpaka hivi sasa kwenye mabaya na mazuri ya maendeleo katika kulitumikia taifa imelalia katika mazuri tena sana. Sasa kwanini ahukumiwe kwa machache mabaya ya kusingiziwa mpaka mfike kuwaita watu wa mataifa ya kigeni kumuazibu? we Lisu angalia sana . Wa kumuadhibu Magufuli kama utendaji wake mbovu ni watanzania peke yake na mpaka wakati muafaka ukifika. Ndio upizani kama kuna watu makini wanaolitakia mema taifa letu wawaonyeshe watanzania udhaifu wa serikali ya Magufuli,yaani waishitaki serikali ya Magufuli kwa watanzania ili wasiipe nafasi nyengine ya kuongoza nchi uchaguzi utakapowadia na sio kuhangaikia nchi ikatiwe misaada yaani huo ni uchawi heavy na ukatili kwa watanzania na hakuna mtu atakaefanya hivyo isipokuwa mtu huyo ana roho mbaya na ukatili wa hali juu kwa nchi yetu . Hayati Abeidi Amani karume Mungu alimjalia kutembea nchi za nje kwa sababu alikuwa baharia. Katika kutembea huko nje alishuhudia mambo mengi sana mbali na maendeleo ya mataifa ya ughaibuni lakini pia dharau aliokuwa akikabiliana nayo kwa kuwa yeye kama mtu mweusi na kwa kuwa anatoka nchi masikini na alipopata nafasi yakuwa raisi wa Zanzibar alizamiria yakuwa wanzanzibar wanaokuja badala yake wakiamua kwenda nchi za nje basi watafanya hivyo kwa ajili ya kwenda kutalii si kufanya kazi na kwa kiasi fulani kutokana na msimamo wake thabiti alishakuwa yupo katika kutimiza ndoto yake hiyo basi wakatokezea watu wa aina ya akina Tundu Lisu wakafanya walioyafanya labda kwa kutumika na mataifa ya nje kwa kujua au bila ya kujua kama wanatumika wakalianzisha dikteta,dikteta basi hayati Karume akakatishwa ndoto yake na Zanzibar yake kwa kuuwawa na laana ile mpaka leo ndio inaoendelea kuitafuna Zanzibar Kwa hivyo sio vyema kurejea kosa .
    Kiasili Magufuli sio wanasiasa ni mtaalamu hakuekeza kuishi maisha yake kwa kupitia siasa ila ameekeza kuishi maisha yake katika kutengeneza kitu, utaona utofauti hapo?

    ReplyDelete
  2. . Kwa bahati mbaya watu wa aina ya Tundu Lisu walitumika au kutumiwa bila ya wao wenyewe kujua kama wanatumika na mataifa ya kigeni hasa ya kibepari ili kuwapinga viongozi ambao wangeliletea Africa mafanikio makubwa ya kimaendeleo. Kwa bahati mbaya kuna baadhi ya viongozi wa Africa waliozamiria kuzikumboa nchi zao juu ya utegemezi wa mataifa ya magharibi walipoteza maisha yao katika mazingira ya kutatanisha aidha kwa kuuwawa kikatili au kupata magonjwa ya kutatanisha. Maadui wasioitakia mema Africa na kutaja demokrasia kama haki za watu lakini kwa upande wa nyuma waliwatumia akina Tundu Lisu kuliangamiza bara la Africa. Kama kweli ni demokrasia basi Egypt au Misri ulifanyika uchaguzi halali na raisi akapatikana halali kabisa bila ya doa lakini kwa kuwa hakuwa raisi anaehitajika na mataifa mabepari raisi huyo akapinduliwa mchana kweupe kabisa na kusekwa gerezani mpaka hivi sasa tunavyozungumza. Hakuna umoja wa mataifa au watu wa haki za binaadamu au mataifa mabingwa wa kulinda demokrasia duniani waliopigia kelele kilichotokea Egypt. Na hayo mataifa makubwa yanayojiita mabingwa wa demokrasia duniani wamekuwa ndio mataifa kipenzi wa raisi wa sasa Egypt ambae hapana shaka hata kidogo yakwamba ni dikteta halisi. Sasa unashangaa sana unapoona watu wanaojiita wasomi kama Tundu Lisu na hata rafiki yake Zitto Kabwe wanapohangaika kuyalimisha mataifa hayo ya kibepari kumuazibu Magufuli na Tanzania yake kisa Uchungu na juhudi anazochukuwa Magufuli kuhakikisha Tanzania inaondokana na umasikini. Kisa jitihada za makusudi za muheshimiwa Magufuli za kuwahamasisha watanzania kufanya kazi kwa bidii baada ya kukaa vibarazani na kuhangaika na mikutano ya kisiasa na kusikiliza ahadi hewa. Hata siku ya hukumu siku ya mwisho ya hesabu mbele ya Mungu Muweza wa kila kitu hakuna kitachosema isipokuwa mizani katika matendo ya mtu. Na Mizani ya muheshimiwa Magufuli mpaka hivi sasa kwenye mabaya na mazuri ya maendeleo katika kulitumikia taifa imelalia katika mazuri tena sana. Sasa kwanini ahukumiwe kwa machache mabaya ya kusingiziwa mpaka mfike kuwaita watu wa mataifa ya kigeni kumuazibu? we Lisu angalia sana . Wa kumuadhibu Magufuli kama utendaji wake mbovu ni watanzania peke yake na mpaka wakati muafaka ukifika. Ndio upizani kama kuna watu makini wanaolitakia mema taifa letu wawaonyeshe watanzania udhaifu wa serikali ya Magufuli,yaani waishitaki serikali ya Magufuli kwa watanzania ili wasiipe nafasi nyengine ya kuongoza nchi uchaguzi utakapowadia na sio kuhangaikia nchi ikatiwe misaada yaani huo ni uchawi heavy na ukatili kwa watanzania na hakuna mtu atakaefanya hivyo isipokuwa mtu huyo ana roho mbaya na ukatili wa hali juu kwa nchi yetu . Hayati Abeidi Amani karume Mungu alimjalia kutembea nchi za nje kwa sababu alikuwa baharia. Katika kutembea huko nje alishuhudia mambo mengi sana mbali na maendeleo ya mataifa ya ughaibuni lakini pia dharau aliokuwa akikabiliana nayo kwa kuwa yeye kama mtu mweusi na kwa kuwa anatoka nchi masikini na alipopata nafasi yakuwa raisi wa Zanzibar alizamiria yakuwa wanzanzibar wanaokuja badala yake wakiamua kwenda nchi za nje basi watafanya hivyo kwa ajili ya kwenda kutalii si kufanya kazi na kwa kiasi fulani kutokana na msimamo wake thabiti alishakuwa yupo katika kutimiza ndoto yake hiyo basi wakatokezea watu wa aina ya akina Tundu Lisu wakafanya walioyafanya labda kwa kutumika na mataifa ya nje kwa kujua au bila ya kujua kama wanatumika wakalianzisha dikteta,dikteta basi hayati Karume akakatishwa ndoto yake na Zanzibar yake kwa kuuwawa na laana ile mpaka leo ndio inaoendelea kuitafuna Zanzibar Kwa hivyo sio vyema kurejea kosa .
    Kiasili Magufuli sio wanasiasa ni mtaalamu hakuekeza kuishi maisha yake kwa kupitia siasa ila ameekeza kuishi maisha yake katika kutengeneza kitu, utaona utofauti hapo?

    ReplyDelete

Top Post Ad