AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe amevunja bodi ya udhamini ya jumuiya matumizi bora ya Maliasili kwa tarafa za Idodi na Pawaga (MBOMIPA) mkoani Iringa kwa kutosaidia wananchi na kufanya kazi kifisadi zaidi pamoja na kuvunja mikataba yote .
Prof Maghembe alifikia uamuzi huo wakati wa ziara yake katika jumuiya hiyo ya MBOMIPA na kufanya mkutano na wajumbe wa Bodi hiyo kabla ya kuvunjwa.
Prof. Maghembe alisema anashangazwa kuona MBOMIPA inajiendesha kwa hasara na kuomba omba kwa wahisani fedha za kujiendesha wakati kimsingi asasi hiyo ilipaswa kuwa msaada mkubwa kwa wanachama wao ambao ni vijiji vinavyozunguka hifadhi hiyo.
“Hii ni aibu kubwa kwa chombo hiki ambacho kinapaswa kuwa msaada kwa jamii chenyewe kimegeuka kuwa ombaomba, hivi inawezekana vipi MBOMIPA kuomba hadi msaada wa sare na mataili mawili kwa wahisani. Hili ni jambo la aibu kifupi halikubaliki hakuna cha mwekezaji hapa wala cha bodi tunaanza upya vitu vyote tunaanza sifuri,” alisema Prof. Maghembe.
“Tutajidanganya kabisa kusema kwamba tuendelee na bodi ya Mbomipa kama ilivyo tutajidanganya kabisa, kwahiyo kuanzia leo nimeivunja bodi ya MBONIPA rasmi leo hapa.”
Aidha Waziri Maghembe ameagiza taasisi ya kuzuia na kupambana na Rushwa nchini (TAKUKURU) kuanza uchunguzi wake na kuwachukulia hatua wote waliohusika na ufisadi katika bodi hiyo ya MBOMIPA.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK