AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (Nemc), limesema wakati wowote litaendesha operesheni ya kubomoa nyumba zote zilizojengwa kando ya Bonde la Mto Msimbazi kinyume cha sheria.
Operesheni hiyo itawahusu pia wale wote waliojenga vibanda katika Bonde la Mkwajuni eneo la Magomeni wilayani Kinondoni.
Akizungumza na wanahabari leo Agosti 28 katika eneo la Mto Msimbazi, Mwanasheria Mwandamizi wa Nemc, Manchare Heche amesema watu wanaoishi katika maeneo hayo wanatakiwa kujiandaa kuondoka katika bonde hilo.
Amesema wanaoishi eneo hilo wanavunja utaratibu kwa kuwa ni sehemu hatarishi kwa maisha yao na kwamba, walishapigwa marufuku lakini baadhi wamerudi kinyemela.
"Mfano hawa wenye vibanda ambavyo vinachomoza kila kukicha katika Bonde la Mkwajuni, tulishawapiga marufuku na hapa palikuwa peupe lakini wamerudi.Sasa nawaambia wajiandae kuondoka hapa, operesheni hii itawahusu,"amesema.
Alipoulizwa bomoabomoa inaanza lini, Heche hakutaka kusema zaidi ya kusisitiza wananchi wajiandae kuondoka ili kupisha operesheni hiyo.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK
Msimbazi mkaanze na ofisi za Mwendokasi hapo jangwani please maana na hapo ni eneo hatarishi....muache dabo std kuwatesa walala hoi
ReplyDelete