Mbaroni kwa Kumpa Mtoto Kinyesi cha Mbuzi

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Mbaroni kwa Kumpa Mtoto Kinyesi cha Mbuzi

JESHI la Polisi Mkoa wa Mwanza, linamshikilia mkazi wa Mtaa wa Chakechake, Sospeter Rajabu (42), kwa kosa la kumpaka kinyesi  cha mbuzi kwenye majeraha yaliyotokana kuungua   moto  mtoto wake, Neema Sospeter (10) mwanafunzi wa darasa la  kwanza na kusababisha hali yake kuwa mbaya.

Taarifa iliyotolewa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Ahmed Msangi jana, ilisema mtuhumiwa  alikamatwa juzi  saa 10:30 jioni  Mtaa wa Chakechake  wilayani  Nyamagana.

Alisema Sospeter anatuhumiwa  kumpaka mavi ya mbuzi  mtoto wake kwenye majeraha ya moto aliyoungua maeneo ya mapaja ya miguu yote miwili kwa muda wa wiki mbili na kusababisha  majeruhi kuwa na hali mbaya kiafya ambapo  wananchi walitoa taarifa polisi kuhusiana na tukio hilo, askari walifanya ufuatiliaji wa haraka hadi maeneo hayo na kufanikiwa kumkuta mtoto akiwa kwenye hali mbaya na  kushirikiana na wananchi kumkimbiza hospitali na  kumkamata baba wa mtoto.

“Huyu mtoto aliungua moto Agosti 4, mwaka huu saa 1:45 usiku  Mtaa wa Kitangiri wilayani Iilemela ambapo alikuwa akiishi na mama yake kwani wazazi wake walitengana kwa muda mrefu, inadaiwa alimwagikiwa na mafuta ya taa alipokuwa akiweka kwenye  kibatari na kuwasha  na njiti ya kibiriti na  moto kulilipuka kisha  kumuunguza.

“Baada ya mama yake  kukosa fedha za matibabu, aliamua kumpeleka  kwa baba yake Mtaa wa Chakechake alipokua akiishi na mke mwingine ili amsaidie mtoto apate matibabu, lakini baada ya mtoto kufikishwa kwa baba yake hakupelekwa hospitali na  badala yake alikuwa akipakwa mavi ya mbuzi na kusababisha  hali yake kuzidi kuwa mbaya,” alisema Kamanda Msangi.

Alisema polisi wapo kwenye upelelezi na mahojiano na mtuhumiwa dhidi ya ukatili aliyokuwa akimtendea mwanae pindi uchunguzi utakapokamilika atafikishwa mahakamani, majeruhi amelazwa Hospitali ya Mkoa wa Mwanza  Sekou Toure akiendelea kupatiwa matibabu na hali yake inaendelea vizuri.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad