Mbunge Prof Jay Afunguka Haya Baada ya Nyumba yake Kukumbwa na Bomoa Bomoa ya Serikali

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Msanii wa hip hop Bongo na Mbunge wa jimbo la Mikumi Joseph Haule ‘Professor Jay’, amezungumzia taarifa za nyumba yake iliyopo Kimara Dar es Salaam kupigwa alama X kama ishara ya kutakiwa kuvunja na kuondoka ili kupisha upanuzi wa barabara.

Rapper huyo mkongwe amesema ni kweli yeye na majirani zake wamewekewa X ila wameungana na serikali ya mtaa, kitongoji, mbunge na diwani kuomba mahakamani kwamba upana tajwa ni mkubwa sana na ni kinyume na utaratibu ambao wanaufahamu wao.

“Wanasema kupanua ni meta 121.5 ni upana mkubwa sana na upande mkubwa sana na watu wengi wataarithirika na wataumia. Kwa sababu tunaamini haki inapatikana mahakamani ndio maana tukaenda kuweka zuio, kuangalia ni jinsi gani tunaweza kupata haki yetu ya msingi lakini kitu kikubwa tunachozidi kusisitiza hakuna mtu anayekataa kuhama kwa ajili ya maendeleo,” Professor Jay ameimbia XXL ya Clouds Fm na kuongeza.

“Wengine tumejenga kwa muda mrefu sana, nakumbuka hii nyumba nimejenga kupitia muziki, unapata lakini mbili unatoa elfu hamsini unanunua misumari halafu laki na nusu unakula bata, kwa hiyo unapoona kwamba inabomolewa kwa siku moja na hakuna fidia serikali inatakiwa iangalia kwa jicho pevu,” amesema Professor Jay.


 Soma Nafasi za Kazi Zilizotangazwa Siku ya Leo Ingia >>www.ajirayako.co.tz
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad