Mkuu wa Wilaya Awasamehe Waliorushia Mawe Msafara Wake

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Mkuu wa Wilaya ya Chemba, Simon Odunga, amewasamehe wanakijiji wa Mlongia kata ya Jongolo waliobeba silaha za

kijadi, virungu na mawe wakidaiwa kuupiga mawe msafara wa Kamati ya

Ulinzi na Usalama wa wilaya hiyo ulipokwenda kutatua mgogoro wa ardhi

katika kijiji hicho.

Akizungumza jana Jumatatu, Odunga amesema ameamua kuwasamehe na kutowafikisha mahakamani wakazi hao wanaodaiwa kuhusika katika vurugu hizo baada ya makubaliano kuwa hawatarudia tena kitendo kama hicho.

“Haina haja ya kuendelea na ugomvi na wananchi ambao unawaongoza.

Niliwasamehe na waliapa kutorudia tena vitendo kama hivyo na sasa hali

imetulia,” amesema Odunga.

Tukio hilo lilitokea Januari mwaka huu wakati Kamati ya Ulinzi na

Usalama ya Wilaya hiyo ilipokuwa ikenda katika mkutano huo uliolenga

kujadili mgogoro wa ardhi kati ya wakazi wa kijiji hicho na mwekezaji

aliyetambulika kwa jina la Msukuma, ambaye anadaiwa kupewa ekari 500

kwa ajili ya kuwekeza katika eneo la kijiji hicho.

Kwa mujibu wa Odunga, hakuna haki ambayo imekiukwa na mwekezaji

huyo bali mvutano huo ulitengenezwa na wanasiasa.

“Hakuna haki ya msingi ambayo imekiukwa katika eneo hilo isipokuwa

mgogoro huo umesababishwa na elimu ndogo na wanasiasa  kuwachochea

wananchi,” alisema.

Alisema kimsingi shamba hilo la mwekezaji lenye ukubwa wa ekari 450 liko katika kijiji cha Kwadelo wilaya ya Kondoa na wala si wilaya ya Chemba.

“Na viongozi wa Wilaya ya Kondoa wanamtambua mwekezaji huyo lakini

wanasiasa hawa wamekuwa wakimpiga vita tangu mwaka 2006, sijui ni

kwa sababu gani,” alisema.

Katika tukio hilo, wanakijiji hao wakiwa na silaha za jadi, mapanga,

virungu na mishale walishambulia Kamati ya Ulinzi na Usalama na

kuharibu pia gari ya Mkuu wa Usalama wa Wilaya baada ya kulipiga mawe.

Tukio hilo lilisababisha watu 30 kukamatwa akiwemo mwenyekiti wa

kijiji na kuhojiwa kuhusiana na fujo hizo
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad