AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
"Anazungumza kama mwanamume halisi," Mayweather, aliyehudhuria sherehe ya kuapishwa kwa Bw Trump mwezi Januari, aliambia tovuti ya Hollywood Unlocked.
Ujumbe wake huo umekosolewa sana, huku baadhi ya wakosoaji wakirejelea visa vya awali ambapo bondia huyo alipatikana na makosa ya kuwadhalilisha wanawake nyumbani kwake.
Bw Trump aliomba rangi kwa matamshi yake hayo ambayo yalikuwa kwenye mkanda wa video uliofichuliwa mwaka jana.
Kwenye video hiyo, Bw Trump anasikika akijitapa kuhusu kuwapiga busu wanawake na kuwakamata kwenye sehemu zao nyeti, wakati wa mazungumzo ya faragha.
Mayweather ameambia Hollywood Unlocked kwamba Bw Trump "hakufanya jambo lolote mbaya".
"Wanaume halisi huzungumza hivi: 'Man, she had a fat ass. You see her ass? I had to squeeze her ass?' (Bwana, ana makalio mazuri. unayaona makalio yake? Ilinibidi kuyafinya makalio yake). "Mwanabondia huyo alisema.
"Kwa hivyo, anapiga gumzo la faraghani. Mazungumzo ya faraghani."
Wengi katika mitandao ya kijamii yalizungumzia historia ya Mayweather ya kuwashambulia wanawake.
Mayweather amewahi kutangaza kumuunga mkono Bw Trump, ambaye wakati mmoja aliwahi kumwelezea kama "mmoja wa mabondia bora zaidi kuwahi kutokea".
Mayweather pia alitetea Bw Trump kuhusu tuhuma za kuunga mkono makundi ya ubaguzi wa rangi.
"Haujawahi kusikia kuhusu Donald Trump kuwa mbaguzi wa rangi hadi alipowania urais," amesema Mayweather.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK