Katika Maisha Hakuna Anayejua Kitatokea Nini Siwezi Kumsema Vibaya Vanessa- Jux

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Katika Maisha Hakuna Anayejua Kitatokea Nini Siwezi Kumsema Vibaya Vanessa- Jux
Mkali wa muziki wa RnB Bongo, Jux amesema ingawa wameachana na Vanessa Mdee siyo sababu ya kumsema vibaya.

Muimbaji huyo ambaye anafanya vizuri na ngoma yake mpya ‘Utaniua’ ameiambia E-Newz ya EATV kuwa analazimika kuwa na nidhamu hiyo kwa sababu kwenye maisha kuna leo na kesho.

“Unajua katika maisha hakuna anayejua kesho kutatokea nini, mimi siwezi kutoa kauli yoyote kwa sababu Vanessa bado nampenda. Tumefanya vitu vingi sana, nampenda na nitaendelea kumpenda kwa kushirikiana kwenye mambo mengi,” amesema Jux.

Katika hatua nyingine alipoulizwa iwapo Vanessa atamfuata na kumtaka warudiane kama atakuwa tayari, Jux alijibu;

“Siwezi nikaliongelea hilo, sijajua kwa hiyo moment itakuwaje, mimi naishi pia siwezi jua kesho nitakutana na nani kitatokea nini, huwezi jua yeye atakutana na nani kitatokea nini, so siwezi nikatoa hilo jibu sasa hivi lakini tuone itakavyokuwa, tunaendelea kuishi you never know,” amesema.

Kipindi cha mapenzi yao waliweza kutoa wimbo wa pamoja uitwao Juu, pia walishirikishwa katika wimbo wa Nikki wa Pili ‘Safari’.



----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad