Madaktari Nchini Kenya Washangaa Tundu Lissu Kuwa Hai

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 Madaktari Nchini Kenya Washangaa Lissu Kuwa Hai
Mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa amesema madakatari nchini Kenya wameshangazwa kumwona Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu akiwa hai kutokana na shambulio la risasi lililotokea Septemba 2017 mjini Dodoma.

Msigwa aliyekuwa miongoni mwa viongozi wa Chadema waliomsafirisha Lissu kutoka Dodoma siku hiyo kwenda jijini Nairobi, aliliambia gazeti hili jana kwamba Lissu alivuja damu nyingi na kama asingepata huduma ya haraka angefariki.

“Tulipofika Nairobi, madaktari walishangaa kuona Lissu akiwa hai, kwa sababu alipoteza damu nyingi sana. Lakini niwashukuru sana madaktari wa hospitali ya Dodoma General kwa huduma waliyotoa kufanya Lissu tufike Nairobi,” amesema Mchungaji Msigwa na kuongeza:

“Nataka tu niwaambie Watanzania kwamba Tundu Lissu wetu aliumizwa sana katika jaribio la kuchukua uhai wake. Watu wasichukulie kama ni jambo dogo, ni jambo kubwa lililoharibu hata akili za watu tuliokuwa karibu naye.”
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad