MCT Kuwashtaki Watakaovunja Uhuru wa Habari

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

MCT Kuwashtaki Watakaovunja Uhuru wa Habari
Baraza la Habari Tanzania  (MCT) limesema litaanza kuwashtaki watakaovunja uhuru wa Habari ikiwamo kuwazuia waandishi wa Habari kupata taarifa, vipigo na matukio yote ya udhalilishaji dhidi yao.

Akizungumza katika Mkutano Mkuu wa MCT, Ofisa Miradi wa Baraza hilo Pili Mtambalike amesema matukio hayo yanaongeza hofu na kuwafanya waandishi  washindwe kutimiza wajibu wao kikamilifu.

Mtambalike amesema pamoja na hatua nyingine wataanza kuwachukulia hatua ikiwamo kuwashtaki wale watakaofanya hivyo huku akiwaasa wanahabari kutoa taarifa vinapotokea vitendo vinavyokiuka uhuru wa habari.

"Tukio likitokea tutalichunguza na tukijiridhisha na tukio linaweza kupelekwa mahakamani tutashtaki," amesema.

Hata hivyo amesema kwa mwaka huu zaidi ya matukio 11 yameripotiwa ikiwamo lile la Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam kuvamia kituo cha  TV cha Clouds.

Rais wa MCT, Jaji Mstaafu Thomas Mihayo amesema baraza hilo lilianzisha Rejista ya  Matukio ya Uvunjaji Haki wa Habari  (PFVR) ili kuhakikisha kila tukio linaripotiwa na kuchukuliwa hatua.

Amesema lengo ni kuhakikisha kunakuwa  na takwimu sahihi za matukio hayo ili wanapowasiliana na Serikali kuwe na mfano halisi.

----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad