Meya Wa Ubungo Kuzungumza Shauri Lake la Vyeti Feki Dhidi ya Makonda Kesho

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Meya Wa Ubungo Kuzungumza Shauri Lake la Vyeti Feki Dhidi ya Makonda Kesho
Meya wa Ubungo (Chadema), Boniface Jacob ameeleza kuwa kesho atafika katika ofisi ya Sekretarieti ya Maadili ya Utumishi wa Umma kuzungumzia shauri lake la vyeti dhidi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam.

Akizungumza na Mwananchi leo Jumatano, Jacob amesema wiki iliyopita amepokea barua kutoka sekretarieti wakimtaarifu kwamba wiki hii ndiyo wanalifanyia kazi shauri lake.

“Wananitaka kwamba baadhi ya mambo niliyoyaongea wananitaka na mimi nipeleke vielelezo vya ufafanuzi lakini kimsingi ni mambo mapya, yaani kana kwamba mtuhumiwa wangu mambo ya vyeti amekiri, amekubali.”

Jacob amesema akitoka kwenye mahojiano hayo na Sekretarieti ya Maadili ataongea na vyombo vya habari juu ya shauri hilo kuhusu kugushi vyeti na malalamiko mengine manne.

Mbali na hilo amesema atazungumzia vishawishi na vitisho katika kulimaliza shauri hilo lisiendelee.

“Kutoridhika na mwenendo wa shauri hilo linavyofanywa kwa kuchelewa na usiri mkubwa sana.”
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad