AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Ijumaa limemfungia kazi na kufanya naye mahojiano moja kwa moja akiwa kwenye studio yake pande za Tegeta jijini Dar na katika makala haya amefunguka mengi likiwemo la kutaka kuolewa na mchumba wake huyo ambaye wapo tofauti kiimani.
Ijumaa: Wanamuziki wengi wamekuwa wakijishauri sana katika suala zima la kubeba ujauzito kutokana na kazi zao, wewe halikukuumiza kichwa hili?
Linah: Kwa sababu niliamua kwa moyo mmoja kabisa wala hilo sikujiuliza hata mara moja kwa kuwa nilitamani mtoto.
Ijumaa: Wakati unaelekea chumba cha kujifungua, muda mfupi kabla ya kuingia uliposti picha ukiwa kwenye uchungu, haikukuletea matatizo hasa kutokana na mila zetu?
Akiwa katika pozi
Linah: Kwanza ile picha sijaiposti nafikiri kulikuwa na mtu pale hospitali na pia haikuwa siku ambayo najifungua ilikuwa ni siku ambayo nilienda kuonana na daktari, sikuwa najisikia vizuri.
Ijumaa: Baba watoto wako yeye sio staa?
Linah: Hapana wala hayuko huko kabisa.
Ijumaa: Sasa mnawezaje kuendana maana mastaa kuna mambo mengi?
Linah: Unajua huyu mchumba wangu alinipenda tangu 2009, ndio kwanza naanza kutoka lakini hakupata muda wa kunifikia hivyo anajua kazi yangu na ndio maana niko nae amekubali kila kitu changu.
Ijumaa: Vipi kuhusu ndoa wewe na mchumba wako kuna matarajio hayo?
Linah: Ndiyo ni hivi karibuni.
Wakiwa na mume wake Shaban
Ijumaa: Lakini mpenzi wako ni Muislam na ninajua wazi kuwa wewe umetoka kwenye familia ya Kikristo inakuaje hili?
Linah: Ni kweli ni Muislam lakini sioni shida kuolewa naye.
Ijumaa: Kipindi cha ujauzito uliweka picha za kuonesha tumbo wazi, hiyo haikuleta shida kwa wakwe zako?
Linah: Namshukuru sana Mungu, nimepata wakwe waelewa sana kikubwa wao wanataka heshima wala hilo la picha hawalitazami.
Ijumaa: Wewe na msanii Amini mlikuwa wapenzi mnaopendana sana, vipi mkikutana sasa hivi?
Linah: Mimi na Amini tunaheshimiana sana kwa kuwa tayari ana mke wake na mimi nina mtu wangu.
Ijumaa: Asante kwa ushirikiano wako
Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.
Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA
Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK