Polisi Lawashikilia Watu Wawili kwa Kukutwa na Dawa za Kulevya

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Polisi Lawashikilia Watu Wawili kwa Kukutwa na Dawa za Kulevya
Jeshi la Polisi Mkoani Mwanza linawashikilia watu wawili kwa kukutwa na dawa za kulevya aina ya mirungi kilo 44  walizokuwa wakisafirisha kutoka Sirali kwenda mwanza kitendo ambacho ni kosa kisheria.

Watu hao wawili waliofahamika kwa majina ya James lawrence (51), mkazi wa Tarime – Mara, amekamatwa akiwa na mirungi kiasi cha kilo 35, aliyokuwa akisafirisha toka Sirali kwenda Mwanza kwenye bus lenye namba T.498 DAK, aina ya Youtong, na Magabe Mirumbe (45), mkazi wa Tarime –Mara, amekutwa na mirungi kiasi cha kilo 09, aliyokuwa akisafirisha kutoka Sirali kwenda Mwanza kwenye bus lenye namba T. 201 DAN aina ya Youtong, jana Septemba 22 majira ya saa mbili usiku.

Taarifa kutoka Jeshi la Polisi Mwanza inasema kuwa askari walikuwa kwenye kizuizi tajwa hapo juu wakisimamisha na kupekua magari yote yaliyokuwa yakipita kwenye barabara ya mwanza kwenda musoma, ili kuweza kubaini madereva na abiria wanaosafirisha madawa ya kulevya. aidha wakati wakiendelea kusimamisha na kupekua magari hayo waliweza kukamata magari tajwa hapo juu yakiwa na abiria hao waliokuwa wakisafirisha mirungi.

Kamanda wa polisi mkoa wa mwanza naibu kamishina wa polisi Ahme Msangi amethibitisha kutkamatawa kwa watu hao na kusema kwamba anatoa wito kwa wakazi wote wa jiji na mkoa wa Mwanza na wamaeneo ya mikoa ya jirani kuacha kujihusisha na biashara haramu ya dawa za kulevya kwani ni kosa la jinai, bali wananchi wafanye kazi halali ya kujipatia kipato na wala sio vinginevyo.
Aidha pia anatoa raia kwa madereva na wamiliki wa mabasi kuacha kusafirisha madawa ya kulevya kwani kosa kisheria.

----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad