AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Mpango huo umezinduliwa leo Jumatatu na Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu ambapo alikabidhi kadi hizo kwa wazee zaidi ya 100 kwa niaba ya wenzao katika viwanja vya Tip -Sinza.
Mwalimu ameeleza kufurahishwa na hatua iliyochukuliwa na Manispaa ya Ubungo kwa kutimiza ahadi ya Rais John Magufuli ya kuweka utaratibu huo wa matibabu bure.
"Nimefurahishwa na hatua hii. Leo natangaza ramsi mmeingia katika rekodi zangu za kuwa manispaa inayowajali wazee. Mimi mwenyewe niwahi kukaa Ubungo wakati nasoma chuo kikuu mlimani nawashukuru sana kwa jambo hili,"amesema Mwalimu.
Amesema wazee wana changamoto mbalimbali ikiwamo kipato kidogo jambo linalosababisha miongoni kushindwa kupata matibabu kwa ufanisi hivyo hatua hiyo itasaidia kupata huduma hizo.
Aliongeza kuwa ni hatua hiyo ni njia ya kuwaelekea katika bima za afya kwa wazee kama mkakati wa Serikali wa kuwasaidia wazee hao.
Mwalimu alitumia nafasi kuwaihidi viongozi wa manispaa ya hiyo atawajengea wodi ya wazazi na chumba cha upasuaji katika mojawapo ya vituo vya afya vya Ubungo.
Meya wa Ubungo, Boniface Jacob amesema manispaa hiyo imejipanga ipasavyo katika kuhakikisha wazee wanapata huduma hiyo ya bure.
"Wengine walizani ni utani, nawaambia sisi hatuna mzaha ndiyo maana leo tumemwita waziri kuja kuzindua. Kauli mbiu yetu ni 'mzee kufa kwa kukosa matibabu sasa basi',"amesema Jacob.w
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK