AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Bomu hilo la tani 1.4 kutoka Uingereza liligunduliwa katika eneo la ujenzi Jumatano.
Habari hizo zilipokelewa kwa shangwe na watu zaidi ya 65,000 ambao walikuwa wamehamishwa maeneo yao kwa sababu za kiusalama baada ya bomu hilo kuteguliwa.
Hiyo ilikuwa idadi kubwa zaidi ya watu kuhamishwa tangu kutokea kwa Vita Vikuu vya Pili vya Dunia nchini Ujerumani, na shughuli hiyo ilihusisha mamia ya maafisa wa serikali.
Maeneo ambayo watu walihamishwa yalikuwa katika mtaa wa Westend, na ni pamoja na hospitali kadha, nyumba za kuwatunza wagonjwa na hata katika Benki Kuu ya Ujerumani.
Inaaminika kwamba kuna mamia ya maelfu ya mabomu ya wakati wa vita ambayo hayakulipuliwa ambayo yametapakaa kote Ujerumani.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK