Massogange Azidi Kukwama Mhakamani Kesi Yake Yasogezwa Mbele

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Massogange Azidi Kukwama Mhakamani Kesi Yake Yasogezwa Mbele
Agnes Gerald maarufu kama ‘Masogange’ amerudi tena kwenye headlines za Mahakamani tena leo October 12, 2017 ambapo hata hivyo, kesi yake ya kutumia dawa za kulevya imesogezwa mbele katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu hadi November 14, 2017.

Masogange alitarajia kuanza kujitetea leo lakini Wakili wa Serikali, Adolf Mkini alimuomba Hakimu Mkazi Mkuu, Wilbard Mashauri aahirishe kesi hiyo hadi tarehe nyingine ambapo kutokana na ombi hilo, Hakimu Mashauri aliahirisha kesi hiyo hadi November 14, 2017.

Masogange ataanza kujitetea baada ya Mahakama kumkuta na kesi ya kujibu kwa upande wa mashtaka ambao ulikuwa na mashahidi watatu.

Masogange anadaiwa kuwa kati ya February 7 na 14, 2017 katika maeneo yasiyojulikana ndani ya jiji la Dar es Salaam alitumia dawa za kulevya aina ya Heroin (Diacety Imophine).

Pia anadaiwa kuwa kati ya February 7 na 14, 2017 alitumia dawa za kulevya aina ya Oxazepam.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad