AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Nyumbu ni kati ya vivutio vinavyoifanya Hifadhi ya Serengeti kuwa kwenye maajabu ya dunia kutokana na jinsi wanavyohama kwa kuvuka Mto Mara kwenda Maasai Mara nchini Kenya na kurudi.
Mkuu wa Kituo cha Utafiti wa Wanyamapori (Tawiri) cha Hifadhi ya Serengeti, Dk Robert Fyumagwa alisema juzi kuwa hali si nzuri.
Dk Fyumagwa alitoa kauli hiyo katika mdahalo wa wadau wa hifadhi ikiwa ni sehemu ya kumbukumbu ya miaka 18 ya kifo cha Mwalimu Julius Nyerere, chini ya uratibu wa Frankfurt Zological Society, Serengeti Media Centre na Chuo cha Utalii (Setco).
“Nyumbu wamepungua kutokana na ujangili wa nyaya unaofanywa na jamii inayozunguka ikolojia hiyo ambayo inasema inamuenzi Mwalimu Nyerere, ikumbukwe yeye alikemea ufujaji wa mali za umma na kila mwananchi ana wajibu wa kulinda maliasili zetu,”alisema.
Meneja wa Mradi wa Frankfurt Zological Society, Masegeri Tumbuya alisema kuwa tangu Aprili hadi Septemba mwaka huu, mitego 6,837 ya nyaya iliteguliwa katika hifadhi ya Taifa ya Serengeti kupitia kitengo maalumu kinachoshughulika na udhibiti wa ujangili huo.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK