Baraka Da Prince: You Tube Akaunti Yangu Inafanyiwa Mchezo Mchafu Ili Ishushe Idadi ya Views

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Baraka Da Prince: You Tube Akaunti Yangu Inafanyiwa Mchezo Mchafu Ili Ishushe Idadi ya Views
Msanii wa muziki wa Bongo Flava, Barakah The Prince amedai kuwa YouTube account yake inafanyiwa mchezo mchafu ili ishusha idadi ya views.

Muimbaji huyo ambaye kwa sasa anafanya vizuri na ngoma yake mpya ‘Sometimes’ ameiambia The Playlist ya Times Fm kuwa views za ngoma yake hiyo zimekuwa zikishuka na kupanda na hata muda mwingine comment kufutwa.

“Kwa upande wa YouTube kuna mchezo mchafu unafanyika kwa sasa hivi, kwa mfano wimbo wangu kama jana ulikuwa ni namba saba kwenye trending ukiangalia video za watu wengine ni namba 40 lakini views wake ni milioni 4.4, nyingine inasoma namba 10 ukiangalia views zake ni laki 5.8 lakini mimi ambayo nina views elfu 20 ninasoma namba saba kwa nini iwe hivyo?” alihoji.

“Kuna mchezo mchafu unafanyika wa ku-block views wangu hata Mx kaniambia kuna mchezo mchafu unafanyika” ameongeza.

Amesema kuwa kuna baadhi ya nchini ikiwemo China mashabiki wake wamekuwa wakilalamika haiwapati video yake lakini video za wa wasanii wengine zinapatikana.

Hata hivyo ameweka wazi kuwa watu wenye access ya kuendesha account yake hiyo ni Mx Carter na Seven Mosha wa RockStar4000 kutokana na makubaliano ya hapo awali, pia ameeleza kuwa yupo katika utaratibu wa kufuta account hiyo na kufungua nyingine.

Ngoma ya Barakah ‘Sometimes’ video yake ilitoka October 28 mwaka huu lakini hivi sasa haipatikani YouTube (imeondolewa).

----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad