HESLB: Hakuna Mwanafunzi Atakayepata Mkopo Wakati Hana Vigezo Staiki

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

HESLB: Hakuna Mwanafunzi Atakayepata Mkopo Wakati Hana Vigezo Staiki
Bodi ya mikopo ya elimu ya juu HESLB imesema hakuna mwanafunzi ambaye atapata mkopo wakati hana vigezo stahiki ambavyo vimeainishwa.

Hayo yamebainishwa leo na Mkurugenzi wa bodi hiyo Abdul Razaq Badru baada ya kuwepo kwa mkanganyiko wa wanafunzi wa mwaka wa kwanza waliokosa mkopo.

“Waombaji waliofika ofisini na wale ambao hawajafika tumesikia malalamiko yao na tunayafanyia kazi lakini mikopo watapata wenye sifa pekee kama huna sifa huwezi kupata mkopo”, amesema Badru.

Aidha Mkurugenzi amesema bajeti ya fedha za mikopo kwa mwaka wa masomo wa 2017/18 ni bilioni 427, kwaajili ya wanafunzi 122,000 wakiwemo wa mwaka wa pili na watatu, huku zaidi ya wanafunzi elfu 30 wa mwaka wa kwanza wakiwa kwenye bajeti ya kupata mkopo.

Badru amesema hadi saa wanafunzi 29,578 tayari wameshapata mikopo kiasi cha shilingi bilioni 96 na wameshaaanza masomo kwasababu walitimiza sifa za kupata mkopo. Amesisitiza kuwa hakuna mwanafunzi atakayekosa mkopo wakati amekidhi vigezo na sifa za kupata mkopo.
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad