AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Mganga Mkuu Hospitali ya Rulenge Sr Goleth Fredrick amesema idadi hiyo imeongezeka baada ya wengine kutolewa katika kituo cha afya Bukiriro na kwamba wanafunzi watatu wamefariki na kufikisha idadi ya vifo vya wanafunzi sita.
Kamanda wa Polisi mkoani Kagera Agustino Olomi amesema chanzo cha wanafunzi hao kujeruhiwa kwa bomu ni baada ya mmoja wao kuliokota akidhani ni chuma chakavu.
“Mmoja wapo aliliokota akidhani kwamba ni chuma chakavu hivyo akaamua kuja nalo shuleni baadaye alipeleke kwa mnunuzi ili aweze kununua madaftari’’amesema
Hata hivyo kamanda wa Kikosi cha Kulinda mipaka cha jeshi la wananchi wa Tanzania JWTZ wilaya ya Ngara meja Mutaguzwa amesema bomu hilo lilikuwa na vipande 36 na lingelipukia ndani ya darasa lingeleta athari zaidi .
Mganga Mkuu wa Hospitali ya Misheni Rulenge, Goreti Francis amethibitisha kupokewa miili ya wanafunzi hao waliopoteza maisha.
“Majeruhi wana majeraha sehemu mbalimbali za mwili, tunafanya kila jitihada kuokoa maisha yao,” amesema Dk Francis.
Akizungumza kwa simu akiwa eneo la tukio, zaidi ya kilomita 50 kutoka Ngara mjini, diwani wa Kibogora, Adronis Bulindoli amesema wanafunzi waliofariki wana umri kati ya miaka minane na tisa.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK