AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Muna ni miongoni mwa wasanii wa filamu zao la Kaole ambaye amejitolea kuwa kama dada wa hiari kwa Lulu, ameonyesha moyo wa kipekee kuliko msanii yeyote Bongo ambapo amekuwa karibu kuanzia siku ya kwanza ya kesi ya Lulu mpaka siku ya hukumu.
Ijumaa limemtafuta Muna na kuzungumza naye mengi juu ya ukaribu huo ambapo amesema kuwa amepokea hukumu ya Lulu ya miaka miwili jela kwa masikitiko makubwa sana lakini kitu anachoamini hilo ni jaribu tu itafika wakati litapita na ataendelea na maisha yake mengine.
Muna akitoka mahakamani baada ya rafiki yake Lulu kuhukumiwa kifungo cha mika miwili jela.
“Unajua mimi namuamini sana Mungu,naamini kabisa hilo ni jaribu na ipo siku litapita na Lulu ataendelea na maisha yake ya zamani kama kawaida,” anasema Muna.
Muna anaongeza kuwa, atakumbuka sana kipindi chote alichokuwa na Lulu, katika mambo mbalimbali waliokuwa wakifanya pamoja kwenye shida na kwenye raha ambapo walipita naye pamoja lakini kubwa atakalolifanya ni kufunga na kumuombea usiku na mchana. “Nitakumbuka nyakati zote nilizokuwa naye pindi yupo uraiani. Kuanzia siku aliopewa huku kazi yangu moja tu sasa kufunga na kuomba kwa ajili yake,” anasema Muna.
Chanzo: Global Publishers
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK