AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Wakati Di Maria akiondoka kwenda PSG hakuna bosi wa United alihangaika kumbembeleza abaki katika timu yao na walionekana walikuwa tayari kumuacha mchezaji huyo aondoke ndani ya muda mfupi.
Imebainikwa kwamba Manchester United walikuwa wakihitaji zaidi mauzo ya jezi ya Di Maria kuliko walivyokuwa wakihitaji uwepo wake katika timu hiyo na hilo lilimkera Muargentina huyo.
Msemaji wa mchezaji huyo amethibitisha kwamba United hawakumhitaji Di Maria ili kushinda makombe na walikuwa wakiambiana kwamba wakimnunua atawasaidia sana katika mauzo ya jezi.
Debora Gomes amesema Di Maria hakuwa na furaha ndani ya United na mabosi hawakuwa na habari naye huku akisema baada ya Fergie kuondoka sasa United imekuwa klabu ambayo haiwazi kuhusu soka tena bali jinsi ya kuingiza pesa tu.
Mwaka 2014 ndio mwaka ambao United walitoa kiasi cha £59m kwa Real Madrid ili kumnunua na inasemekana hadi anaondoka United walishauza jezi za Di Maria ambazo ziliwaingizia zaidi ya £75m.
Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.
Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA
Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK