Manchester United Hawakuwa Wakimhitaji Di Maria Bali Waliitaka Jezi yake tu

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Kati ya usajili ambao Luis Van Gaal aliufanya na ukawa gumzo dunia nzima ilikuwa ni usajili wa Angel Di Maria kutoka Real Madrid ambaye baada ya msimu mmoja tu waliamua kuachana naye akaenda PSG.

Wakati Di Maria akiondoka kwenda PSG hakuna bosi wa United alihangaika kumbembeleza abaki katika timu yao na walionekana walikuwa tayari kumuacha mchezaji huyo aondoke ndani ya muda mfupi.

Imebainikwa kwamba Manchester United walikuwa wakihitaji zaidi mauzo ya jezi ya Di Maria kuliko walivyokuwa wakihitaji uwepo wake katika timu hiyo na hilo lilimkera Muargentina huyo.

Msemaji wa mchezaji huyo amethibitisha kwamba United hawakumhitaji Di Maria ili kushinda makombe na walikuwa wakiambiana kwamba wakimnunua atawasaidia sana katika mauzo ya jezi.

Debora Gomes amesema Di Maria hakuwa na furaha ndani ya United na mabosi hawakuwa na habari naye huku akisema baada ya Fergie kuondoka sasa United imekuwa klabu ambayo haiwazi kuhusu soka tena bali jinsi ya kuingiza pesa tu.

Mwaka 2014 ndio mwaka ambao United walitoa kiasi cha £59m kwa Real Madrid ili kumnunua na inasemekana hadi anaondoka United walishauza jezi za Di Maria ambazo ziliwaingizia zaidi ya £75m.
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad