Mfanyabiashara Akamatwa na Kilo Nane za Dhahabu Uwanja wa Ndege

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Mfanyabiashara Akamatwa na Kilo Nane za Dhahabu Uwanja wa Ndege
Mfanyabiashara, Naushad Mohamed Suleiman amekamatwa katika Uwanja wa Ndege Zanzibar alikokuwa asafirishe kilo nane za dhahabu.

Pia amekutwa na fedha taslimu za mataifa 15.

Kaimu Kamishna wa Polisi Zanzibar, Juma Yussuf Ali amesema leo Alhamisi Novemba 30,2017 kuwa, mtuhumiwa alikamatwa jana Jumatano Novemba 29,2017 saa tatu usiku akitaka kusafiri na ndege ya Fly Dubai.

Amesema miongoni mwa fedha alizokutwa nazo ni dola 235,000 za Marekani na euro 57,000.

Juma amesema mfanyabiashara huyo alikamatwa baada ya upekuzi kufanyika kwenye mizigo yake.

Amesema ili kusafirisha madini na fedha ni lazima kuwa na vibali kutoka mamlaka husika ndiyo maana wanamshikilia na itakapobainika hakuna utaratibu uliokiukwa ataachiwa.

Juma amesema kazi ya polisi ni kufanya mahojiano na mtuhumiwa.
Chanzo: Mwananchi
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad