Mshambuliaji wa Azam FC Waziri Junior Apata Pigo Mama Yake Mzazi Afariki Dunia

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Mshambuliaji wa Azam FC Waziri Junior Apata Pigo Mama Yake Mzazi Afariki Dunia
Mshambuliaji wa klabu ya soka ya Azam FC Wazir Junior amefiwa na mama yake mzazi usiku wa kuamkia leo nyumbani kwao wilayani Lushoto mkoani Tanga.

Taarifa kutoka klabu hiyo zimethibitisha msiba huo ambapo tayari mchezaji huyo amepewa ruhusa ya kwenda nyumbani kwaajili ya kushiriki msiba huo wa mama yake.
Klabu ya Azam FC imepokea kwa masikito makubwa msiba huo mzito wa mama yake Wazir hivyo imeungana na familia nzima kwenye kipindi hiki kigumu.
Wazir alikuwa amesafiri na timu kuelekea Njombe kwaajili ya mchezo wa ligi wikiendi hii dhidi ya Njombe Mji lakini tayari ameenza safari ya kurejea Dar es salaam asubuhi hii ambapo ataunganisha hadi Lushoto Tanga.
Uongozi wa Azam FC kwa niaba ya mashabiki na klabu kwa ujumla, umetoa salamu za rambirambi kwa ndugu, jamaa na marafiki pamoja na familia ya Junior.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad