AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Baadhi ya nyota wanaoonekana kukalia kuti kavu kwa kuzingatia sababu zilizotolewa na Omog ni pamoja na majeruhi Saidi Mohammed (kipa), Shomari Kapombe (beki) na straika Nicholas Gyan ambaye ameshindwa kuonyesha makali yake kama alivyokuwa kwao Ghana.
Omog aliliambia gazeti hili kuwa anatarajia kukutana na viongozi wa Simba mwishoni mwa wiki ili kuwasilisha mapendekezo yake ambayo yanalenga kuimarisha kikosi chake.
"Tutakuwa na kikao na viongozi wikendi hii, sisemi ni idara gani ninataka kuiimarisha, lakini kwanza nitaanza na wachezaji ambao hawajaonyesha viwango vizuri na wale majeruhi wa muda mrefu," alisema Omog.
Alisema kuwa mbali na kusaka ubingwa wa Ligi Kuu Bara, Simba inayodhaminiwa na Kampuni ya Kubahatisha ya Matokeo Michezoni ya SportPesa, inatakiwa pia ifanye vizuri katika mashindano ya Kombe la FA na michuano ya kimataifa ya Kombe la Shirikisho Afrika watakayoshiriki kuanzia mapema Februari mwakani.
"Tunatakiwa tuwe imara kila idara, tunaelekea kwenye hatua ngumu zaidi, tunahitaji kuwa na wachezaji ambao wanauwezo na uzoefu wa kuisaidia timu," Omog aliongeza.
Dirisha dogo la usajili lililofunguliwa tangu Novemba 15 na litafungwa ifikapo Desemba 15, mwaka huu, siku chache kabla ya Yanga na Simba zitakazochuana kwenye mashindano ya CAF kutakiwa kupeleka majina ya nyota wake iliyowasajili.
Simba ambayo msimu huu imefanikiwa kuondoka na pointi sita Mbeya, inaendelea na mazoezi kwa ajili ya kuwakaribisha Lipuli FC katika mechi ya Ligi Kuu itakayopigwa Jumapili kwenye Uwanja wa Azam Complex uliyopo Chamazi jijini Dar es Salaam.
Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.
Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA
Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK