Rooney Afunga Goli la Mwaka Asema Hakuwai Kufunga Bao Kama Hilo Katika Maisha Yake ya Soka

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Rooney Afunga Goli la Mwaka Asema Hakuwai Kufunga Bao Kama Hilo Katika Maisha Yake ya Soka
Wayne Rooney amesema bao alilofunga dhidi ya West Ham United litabaki katika kumbukumbu yake daima.

Rooney alisema hakuwahi kufunga bao maridadi katika maisha yake ya soka tangu alipoanza kucheza soka Everton, Manchester United na timu ya taifa ya England.

Nahodha huyo wa zamani wa Man United na England aliiongoza Everton kupata ushindi mnono wa mabao 4-0 ikiwa nyumbani kwenye Uwanja wa Goodison Park.

Nguli huyo alifunga mabao matatu ‘hat trick’ kwa mara ya kwanza tangu aliporejea Everton katika usajili wa majira ya kiangazi kutoka Man United.

Pia ushindi wa Everton ni ukaribisho wa kocha mpya Sam Allardyce ‘Big Sam’ aliyetua Goodison Park baada ya kuwa nje ya uwanja muda mrefu tangu alipojiuzulu kuinoa England.

Rooney alifunga bao la kwanza kwa shuti kali akiwa katikati ya uwanja dakika ya 66 akimtungua kipa mkongwe Joe Hart umbali wa mita 54.

“Hili ni bao bora zaidi kati ya mabao yangu niliyowahi kufunga. Ni mara ya kwanza kufunga ‘hat trick’ nikiwa Everton ni hili ndilo bao maridadi tangu nilipoanza kucheza soka,”alisema Rooney.

Mbali na kufunga mabao hayo, Rooney mwenye miaka 32 alikuwa nahodha katika mchezo huo na alicheza kwa kiwango bora dakika zote 90.

Pia alidokeza alifunga bao zuri kwa mkwaju wa penalti kwa kuwa anatambua udhaifu wa Hart tangu wakiwa wote timu ya taifa.

“Bao la kwanza lilikuwa muhimu. Nimejifunza sana kupiga penalti nyingi dhidi ya Joe Hart na najua jinsi ya kumfunga kwa kuwa anajua udhaifu wake,” alisema Rooney.

Matokeo hayo yamemuweka David Moyes katika mazingira magumu na juzi alichukizwa na kiwango cha wachezaji wake akidai walicheza ovyo na walistahili kufungwa.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad