Tanesco Yaanza Kuhamisha Mali Zake Kwenye Jengo Lao Lililowekwa X

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Tanesco Yaanza Kuhamisha Mali Zake Kwenye Jengo Lao Lililowekwa X
Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) linahamisha mali zake kwenye jengo linalopaswa kubomolewa eneo la Ubungo lililo ndani ya hifadhi ya barabara.

Pilikapilika za wafanyakazi wa shirika hilo kuhamisha mali zinaendelea leo Jumanne Novemba 28,2017.

Kaimu Meneja Uhusiano wa Tanesco, Leila Muhaji amesema wanahamia katika ofisi zingine za shirika hilo zilizoko jijini Dar es Salaam.

Uongozi wa Tanesco katika taarifa kwa umma iliyotolewa jana Jumatatu Novemba 27,2017 ulisema umeanza utekelezaji wa agizo la Rais John Magufuli kuhusu kubomolewa jengo hilo.

Novemba 15,2017 akitokea Chato alipokwenda kwa mapumziko baada ya ziara ya Uganda, Rais Magufuli aliagiza Wakala wa Barabara Tanzania (Tanroads) kuweka alama ya X katika jengo lenye ofisi za Tanesco sehemu zilizo katika hifadhi ya barabara.

Tanesco imeanza kubomoa ukuta wa mbele ya jengo hilo na kuhamisha watumishi kupisha shughuli za ubomoaji kufanyika kwa usalama.

Uongozi wa shirika hilo na Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) unaendelea kufanya utaratibu utakaowezesha ubomoaji wa jengo hilo la ghorofa kufanyika bila kuathiri huduma kwa wateja wa Tanesco.

“Katika kipindi hiki cha utekelezaji wa agizo la Rais. Tunapenda kuwahakikishia wateja  na Watanzania kwa jumla kuwa, huduma za umeme zitaendelea kupatikana kama kawaida ikiwemo huduma ya ununuzi wa Luku,” imesema taarifa hiyo.
Chanzo: Mwananchi
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad