Waziri wa Maji Afunguka Kuhusu Bomoabomoa 'Sitaondoka Mpaka Majengo Yote Yabomolewe Leo Lazima Majengo Yawe Chini'

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Waziri wa Maji Afunguka Kuhusu Bomoabomoa 'Sitaondoka Mpaka Majengo Yote Yabomolewe Leo Lazima Majengo Yawe Chini'
Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Mhandisi Isack Kamwelwe amesema ametoka Dodoma kuja Dar es Salaam kusimamia ubomoaji wa majengo ya ofisi za wizara kupisha upanuzi wa barabara.

Kamwelwe amesema leo Jumatatu Novemba 27,2017 kuwa hatua hiyo ni utekelezaji wa agizo la Rais John Magufuli na kupisha ujenzi wa barabara pana inayokwenda Chalinze mkoani Pwani.

Amesema atahakikisha majengo yote yaliyo ndani ya hifadhi ya barabara yanabomolewa leo.

Waziri amesema watendaji wake wamejipanga na ofisi yake tayari ilishahamia Dodoma.

"Nimekuja juzi kutoka Dodoma kuja kusimamia ubomoaji wa majengo haya ya Serikali. Jana tumekaa mpaka saa mbili usiku na kukubaliana kwamba leo lazima tubomoe," amesema waziri.

Amesema tayari wananchi wameshabomolewa nyumba kupisha ujenzi wa barabara, hivyo Serikali nayo ni lazima itimize wajibu wake kwa kubomoa majengo yake kama inavyotakiwa.

"Sitaondoka mpaka majengo yote yabomolewe. Ninachotaka leo lazima majengo yawe chini," amesema Kamwelwe.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad