AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Tukio hilo lilishuhudiwa na paparazi wetu mapema wiki hii ambapo mrembo huyo alinaswa akikatiza mitaa ya Bamaga-Mwenge kuelekea Sayansi akiwa ameongozana na bwa’mdogo mmoja ambaye jina lake halikufahamika mara moja.
Watu waliokuwa kwenye magari yao binafsi walionekana kupunguza mwendo na kumfuatilia Kajala kwa karibu huku wale makondakta wakipiga miluzi kutokana na jinsi walivyopagawa na mrembo huyo.
“Oyooo dah hawa watu nilidhani ni mambo ya kwenye TV kumbe ukiwaona laivu pia ni balaa,” alisikika konda mmoja aliyekuwa kituoni Bamaga.
Paparazi wetu alimfuatilia hatua kwa hatua Kajala ambapo baadhi ya wenye magari binafsi walionekana wanataka kusimama kabisa, lakini walionekana kushindwa kufanya hivyo wakimhofia kijana ambaye aliongozana na Kajala.
“Unaweza kukuta huyo mshikaji japo anaonekana mdogomdogo lakini anatoka na Kajala. Hawa mastaa hawashindwi hawa,” alisikika jamaa mmoja aliyekuwa akimkodolea macho Kajala.
Njemba mwingine alisikika akisema kuwa; “Mh! Kajala huyu si yule wa mwanzo. Amebongeka sana. Kwa kweli hili umbo lake kwa sasa hastahili kutembea kwa miguu kama hivi. Huyu ni mtu wa kukaa kwenye gari muda wote.”
Mwanahabari wetu aliendelea kumfuatilia Kajala kwa muda mrefu, lakini baadaye alibaini kuwa yupo mazoezini kwani alikuwa akienda na kurudi na hata alivyomshtukia paparazi wetu akimfotoa picha, hakutaka kuzungumzia lolote.
Chanzo: Global Publishers
Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.
Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA
Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK