AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Shibuda ameomba hilo leo Disemba 18, 2017 akiwa kwenye Mkutano Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na kusema endapo Rais akiwasaidia milioni 20 kwa kila jimbo hivyo wataweza kushiriki uchaguzi wa marudio wa Ubunge katika majimbo matatu ambao unategemewa kufanyika Januari 13, 2018.
"Nakuomba utombee kwa Rais wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli atutazame tupate ruzuku vyama visivyo pata ruzuku ili tuwe sawa na wale unaowapa ruzuku lakini hawapendi kushiriki katika masuala ya uzalendo na utaifa, lakini chonde chonde nakuomba utuombee" alisema Shibuda
Baada ya maombi yake hayo Rais Magufuli alimuuliza kama yeye na chama chake atashiriki katika uchaguzi wa marudio wa wabunge ndipo hapo aliporudi na kuomba apewe milioni 20 kwa kila jimbo.
"Naomba nisaidie milioni 20 kwa kila jimbo ili niwezeshe kwenda kugombea kwa hiyo kwa majimbo matatu tusaidie chama milioni 60 kwa sababu unaowapatika ruzuku hawakwenda kushiriki" alisisitiza Shibuda.
Baadhi ya Vyama vya siasa vya upinzani nchini Tanzania kikiwepo CHADEMA, CUF, TLP, CHAUMMA pamoja na ACT Wazalendo vimejitoa kushiriki katika uchaguzi mdogo wa marudio wa nafasi ya Ubunge ambao unategemewa kufanyika Januari 13, 2018 kwa kile walichodai kuwa uchaguzi wa madiwani uliofanyika karibuni haukuwa wa haki na ulitawaliwa na uvunjwaji wa haki za binadamu na kanuni za uchaguzi.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK