Mbunge Kuanzisha Darasa la Viazi Lishe

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Mbunge Kuanzisha Darasa la Viazi Lishe
 Ili kukabiliana na changamoto ya utapiamlo na lishe duni wananchi wametakiwa kuweka nguvu katika kilimo cha viazi lishe.

Takwimu zinaonyesha tatizo la lishe duni ni changamoto nchini na asilimia 30 ya Watanzania wakiwemo watoto wanakumbana na tatizo hilo.

Mbunge wa Mkinga, Dunstan Kitandula amesema hayo leo Jumamosi Desemba 16,2017 akipokea mbegu za viazi lishe kutoka Taasisi ya Utafiti wa Kilimo ya Ukiriguru.

Kitandula ambaye pia ni mwenyekiti wa wabunge wahamasishaji wa masuala ya lishe amesema amechukua mbegu hizo kwa ajili ya kuanzisha shamba darasa jimboni kwake atakalolitumia kuwafundisha wananchi umuhimu na namna ya kulima zao hilo.

Amesema ni ajabu kuoana ukosefu wa lishe unaendelea kuwasumbua watoto wakati viazi lishe vinaweza kutumika kama dawa ya kukabiliana na hali hiyo.

“Serikali inajitahidi kukabiliana na changamoto hii lakini naona bado na sisi kama wabunge tuna jukumu la kuingilia kati na kutoa elimu kwa wananchi,” amesema.

Amesema wamezungumza na jukwaa la wadau wa kilimo (Ansaf) ambalo limekubali kuwezesha upatikanaji wa mbegu na wabunge watakwenda kupanda katika majimbo yao ili kusambaza elimu.

Kitandula ni miongoni mwa wabunge waliowezeshwa kupata mbegu na Ansaf. Mwingine ni Mbunge wa Urambo, Margaret Sitta.

“Hakuna sababu ya kuendelea kuwa na watu wenye utapiamlo, tutahamasisha viazi hivi vilimwe hata shuleni ili changamoto ya chakula kwa wanafunzi itatuliwe,” amesema.

Amesema eka moja ya viazi lishe ina uwezo wa kumpatia mkulima kati ya Sh15 milioni na Sh20 milioni.

Mtafiti kutoka taasisi ya Ukiriguru, Erick Chang’a amesema tafiti za kisayansi zinaendelea na zimepatikana mbegu bora za viazi lishe zinazostahimili magonjwa.

Amezitaja aina ya mbegu za viazi lishe ambazo zimeonekana kuwa na matokeo bora zaidi ni kabode, kakamega na mataya.

Amesema, “Licha ya kuwa vinaingiza fedha kwa wale wanaofanya kilimo cha biashara viazi lishe ni vizuri kwa wajawazito na ni chanzo kikubwa cha vitamini A ambayo inasaidia uwezo wa macho kuona na kuifanya ngozi kuwa nzuri.”


----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad