Nauli Mabasi ya Mkoani Pasua Kichwa Yapandishwa Kinyemela

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Nauli Mabasi ya Mkoani Pasua Kichwa Yapandishwa Kinyemela
Nauli za mabasi yaendayo mikoani katika stendi kuu ya Ubungo zimebainika kupandishwa kinyemela tofauti na bei elekezi iliyotolewa na Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Majini na Nchi Kavu (Sumatra).

Mwenyekiti wa bodi ya Sumatra Dk John Ndunguru jana alitembelea stendi hiyo na kukagua namna abiria wanavyohudumiwa hasa kipindi hiki cha kuelekea sikukuu za mwisho wa mwaka.

Katika ukaguzi uliofanyika, baadhi ya mabasi yamekamatwa likiwamo linalofanya safari za Dar es salaam na Arusha kwa kuongeza nauli kinyume na ilivyopangwa na Sumatra.

Dk Ndunguru alisema changamoto ni nyingi hasa magari ya kanda ya ziwa yamekuwa yakichezewa vidhibiti mwendo vilivyofungwa.

“Changamoto ipo kwa magari ya kaskazini mtu anayekwenda Same, Mwanga na Moshi nauli yake ni Sh22,500 lakini wapo wanaotozwa Sh35,000. Nawaagiza makamanda kuwafuatilia wote na kuwafikisha kituoni,” alisema Dk Ndunguru.

Dereva wa basi la Saratoga linalofanya safari zake Dar es salaam na Mwanza ameilalamikia Sumatra akisema kuna mabasi mengine yanayotoa huduma lakini hayajafungwa vidhibiti mwendo jambo ambalo si sawa.

Beatrice Pendaeli abiria anayesafiri kuelekea Arusha amewataka Sumatra wawe wanafanya ukaguzi wasingoje siku za sikukuu pamoja na kuwachunguza wanaokata tiketi ili kudhibiti feki.

Kamanda wa Polisi kikosi cha usalama barabarani mkoa wa Kinondoni, Saimon Mwangamilo alisema kwa kipindi hiki cha mwisho wa mwaka watu wengi wanakwenda mapumziko huku baadhi ya mawakala wakipandisha nauli kinyemela.

“Jeshi la polisi tumejipanga vizuri, tutahakikisha kipindi hiki cha sikukuu za mwisho wa mwaka tunawakamata mawakala wote watakaopandisha nauli pamoja na kuwafikisha mahakamani,” alisema Mwangamilo.

Pia, aliwashauri wasafiri kukata tiketi kwenye vituo vya mabasi husika badala ya kuwatumia wapigadebe ambao wanapandisha nauli na wengine wanatumia vitabu feki vya tiketi.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad