Raila Odinga Asema Yupo Tayari Kufa

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Raila Odinga Asema Yupo Tayari Kufa
Kiongozi wa upinzani nchini Kenya kupitia NASA, Raila Omolo Odinga, amesema yupo tayari kufa ikiwa ndiyo gharama atakayolipa baada ya kuapishwa kama rais wa wananchi, lakini lazima haki itendeke.


Raila Odinga ametoa kauli hiyo alipokuwa kwenye mazishi ya Mbunge wa nchi hiyo Francis Nyenze katika eneo la Kitui, na kueleza kwamba ataapishwa kuwa rais hata kama itamgharimu hukumu ya kifo kwa kufanya hivyo.

"Iwapo kifo ndio gharama ambayo lazima tuilipe kwa haki ya uchaguzi Kenya, na kwamba hakutakuwa na dhuluma za uchaguzi tena baadaye, tupo tayari kulipa hiyo gharama, tutaapishwa na wafanye kile wanataka kufanya", alisikika Raila Odinga.

Odinga aliendelea kwa kusema kwamba alishinda uchaguzi wa Agosti 2017 ambao ulifutwa na Mahakama ya Juu, na kuapa kuendelea kupambana kuleta mabadiliko katika uongozi wa nchi.

"Tulisema tulishindauchaguzi na tutaapishwa, tumeonywa kwa hukumu na kifo, nataka nimwambie Githu Muigai (Mwanasheria Mkuu wa Kenya) na bosi wake, tutaapishwa na tutaufa", amesema Odinga.

Hivi karibuni Mwanasheri aMKuu wa Kenya amemuonya Raila Odinga kuendelea na mpango wake wa kujiapisha wakati tayari kuna Rais aliyeapishwa kwa mujibu wa katiba ya nchi hiyo, na kusema kwamba sheria itachukua mkondo wake.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad