Viongozi wa Chadema Watinga Mahakamani Leo Katika Kesi ya Lijuakali, Susan Kiwanga

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 Viongozi wa Chadema Watinga Mahakamani Leo Katika Kesi ya Lijuakali, Susan Kiwanga
Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe na mjumbe wa kamati kuu ya chama hicho, Frederick Sumaye, wamehudhuria katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Morogoro ambako uamuzi wa dhamana ya wanachama wa chama hicho utatolewa.

Wengine waliofika mahakamani ni mbunge wa Tarime Vijijini, John Heche na wa Viti Maalumu, Devota Minja.

Wabunge Susan Kiwanga na Peter Lijualikali wamefikishwa katika Mahakama hiyo leo Jumanne Desemba 5,2017 kusikiliza uamuzi wa dhamana yao pamoja washtakiwa wengine 36.

Kesi hiyo ipo mbele ya hakimu Ivan Msack. Ulinzi umeimarishwa ndani na nje ya Mahakama, huku barabara zote zinazoelekea mahakamani zikiwa zimefungwa.

Washtakiwa wanatetewa na mawakili Peter Kibatala, Ignas Punge, Fredrick Kiwelo na Bartholomew Tarimo.

Upande wa mashtaka unawakilishwa na mawakili wa Serikali, Edga Bantulaki na Sunday Hyera.

Washtakiwa wanakabiliwa na mashtaka manane likiwemo la kuchoma moto ofisi ya Kata ya Sofi iliyopo wilayani Malinyi.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad