Kocha Simba Sc Amtolea ‘Povu’ Mavugo

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Kocha Simba Sc Amtolea ‘Povu’ Mavugo
KOCHA Msaidizi wa Simba, Masoud Djuma amesema kuwa ushindi ambao timu yake iliyoupata jana Alhamisi katika mchezo dhidi ya Singida United ulichangiwa kwa kiasi kikubwa na mabadiliko ya wachezaji wake huku akimtolea ‘povu’ straika wale Laudit Mavugo.

Simba ilipata ushindi wa mabao 4-0 katika mchezo wa Ligi kuu Bara kwenye Uwanja wa Taifa dhidi ya wababe hao wa Singida ambapo mabao yake yalifungwa na Shiza Kichuya, Asante Kwasi na Emmanuel Okwi aliyefunga mawili. Akizungumza mara baada ya mchezo huo, Djuma alisema nafasi ya Okwi kucheza ilitakiwa ichukuliwe na Mavugo lakini kwa kuwa

Mavugo hakuonyesha kiwango kizuri mazoezini ilimbidi afanye mabadiliko hayo. “Okwi amefanya mazoezi na sisi siku mbili tu kama mnavyojua hakuwepo kambini, nilipanga kumtumia Mavugo lakini nimemwambia kuwa hakuonyesha uwezo mzuri, ndiyo maana nikaamua kumpa nafasi Okwi na kweli ameitumia vizuri. “Nimeshamueleza Mavugo kuwa yeye ni ndugu yangu lakini katika hili suala la kazi anatakiwa kuonyesha uwezo na kufanya kweli, siwezi kumpa nafasi kama haonyeshi uwezo,” alisema kocha huyo.

KUHUSU KOCHA MPYA

Kuhusu kocha mpya wa Simba, Pierre Lechantre raia wa Ufaransa aliyekuwepo jukwaani akifuatilia mchezo huo, Djuma alisema yeye hana tatizo na ujio wa kocha huyo, anamkaribisha na yupo tayari ku- fanya naye kazi. “Nipo tayari wala sina tatizo, namkaribisha na tutakuwa pamoja, kuhusu mfumo na maendeleo mengine nitampatia ripoti kisha yeye ndiye atakayeamua juu ya kutumia au la,” alisema. Upande wa Kocha wa Singida United, Hans van Pluijm alisema matokeo ya mchezo huo yametokana na walinzi wake kufanya makosa na Simba wakayatumia vizuri.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad