"Sholo Mwamba ni Mfa Maji"- Man Fongo''

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

"Sholo Mwamba ni Mfa Maji"- Man Fongo
Msanii wa miondoko ya singeli Man Fongo amesema hawezi kukaa na kumzungumzia Sholo Mwamba kwa madai yeye ni mfa maji ndiyo maana haishi kutapa tapa kila uchao kumtaja.


Man Fongo ameeleza hayo baada ya masaa machache kupita tokea kuonekana kwa 'video' ya Sholo iliyorushwa na EATV katika kipindi cha 'FRIDAY NIGHT LIVE' (FNL) usiku wa kuamkia leo, ikiwa imemuonyesha akimlaumu msanii mwenzake kuwa hana kipaji cha kuendelea kufanya muziki mzuri ndani ya mwaka 2018 huku akimtaka arejee katika fani yake ya awali ya 'DJ'.

"Mimi kwa sasa siwezi kumzungumzia mtu yeyote kwa maana naangalia muziki wangu kwa sababu ndiyo unaonifanya nieleweke kwa wadau wangu, pia unasababisha familia yangu ipate kula. Kwa hiyo mtu akitaka kutoka kwa kutumia kiki na kupitia mgongo wangu nakuwa bado simuelewi. Hivyo siwezi kumtumikia Sholo Mwamba 'eti aniambie mimi nirudi katika fani yangu ya 'DJ' wakati yeye hayupo katika 'manegement' yangu na yeye ni msanii kama mimi", alisema Man Fongo wakati alipofanyiwa mahojiano maalum.

Pamoja na hayo, Man Fongo ameendelea kwa kusema "ninachopenda kumshauri Sholo Mwamba ni kwamba atoe ngoma mpya ili aweze kusikilizwa na raia anachokifanya, apambanie muziki wake aweze kufika mbali na asiangalie muziki wangu mimi", alisisitiza Man Fongo.

Kwa upande mwingine Man Fongo amesema mwaka 2018 amejiandaa vizuri katika ufanyaji kazi wake na wala haiwezi kuwa kama alivyosema mpinzani wake huyo ambae kwa muda mrefu wamekuwa wakitoleana mapovu katika vyombo vya habari na mitandao ya kijamii.

"Kazi mpya nimeangusha juzi tu na mpaka sasa ninapo kwambia inafanya vizuri hivyo Sholo Mwamba ni mfa maji tu kama mtu ambae anatapa tapa yaani mfa maji haishi kutapa tapa. Kwa hiyo ameona bora apate kiki kwa mgongo wangu ili aweze kutoka", alisema Man Fongo.
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad