AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Picha inayohusiana
Rais Jacob Zuma akiwa na baadhi ya wanafamilia ya kifahari ya GUPTA.
Kwa mujibu wa mtandao wa Reuters umedai kuwa polisi wamezingira barabara zote zinazoingia kwenye eneo la nyumba za familia hiyo huku wakiwa na silaha nzito za kijeshi.
Msemaji wa jeshi la polisi mjini Johannesburg, Hangwani Mulaudzi amethibitisha taarifa hiza lakini amekataa kutolea maelezo kwa nini nyumba hiyo ya kifahari imezingirwa na polisi.
Tangu mwaka 20015 familia ya Gupta imekuwa ikishutumiwa na viongozi wa upinzani nchini Afrika Kusini kuwa inahifadhi mali za wizi zinazoibwa serikalini na Rais Zuma.
Ulinzi huo umekuja katika kipindi hiki ambacho Chama cha ANC kwa sauti moja kimetoa tamko la kumshinikiza Rais Jacob Zuma kujiuzulu nafasi yake ya urais.
Jana chama hicho kilimpa masaa 48 Rais Jacob Zuma kujiuzulu urais huku mwenyewe akitaka apewe muda wa miezi mitatu hadi sita kuchukua uamuzi huo.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK