AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Waziri Mwakyembe alisema Uwanja wa Taifa utatumika kwaajili ya ufunguzi na kufungukia mashindano hayo, huku viwanja vingine vya Uhuru na Azam Complex Chamazi vikitumika katika mechi za mashindano hayo.
"Tunataka tufanye mabadiliko katika hizi nyasi bandia za uhuru tuweke mpya, lakini uwanja wa Gymkhana utatumika kwa mazoezi, bado kuna viwanja vingine tunaendelea kuvichagua ili timu zipate sehemu ya kufanyia mazoezi kwa urahisi," alisema Mwakyembe.
Waziri Mwakyembe alisema wanajua wingi wa timu nane zinazokuja zitakuwa na viongozi, wachezaji na mashabiki hivyo wanajiandaa kuhakikisha wageni hao wanapata mahitaji yao mapema.
"Magari yanahitajika kwaajili ya kuwabeba wageni wetu hivyo inabidi yapatikane na kuandaliwa mapema, lakini pia tunajupanga juu ya suala la foleni wasiweze kukutana nalo,'' alisema.
Mwakyembe aliongeza kwamba wanaendelea na maandalizi, wapo katika hatua nzuri kwa ajili ya mashindano hayo.
Mwananchi
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK