AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
KENYA: Kiongozi wa wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Meru, Evans Njoroge ameuawa kwa kupigwa risasi na Polisi jana Februari 27, 2018 katika maanadamano chuoni hapo
-
Wanafunzi hao waliandamana wakishinikiza Chuo hicho kupunguza ada kwa kiasi cha shilingi 8,500 za Kenya ambazo ni sawa na Tsh 188,566 na kuboreshewa miundombinu chuoni hapo
-
Mashuhuda wa tukio hilo wamesema kuwa wanafunzi wa Chuo hicho baada ya vurugu walikimbia nje ya chuo na kwenda kujificha mashambani baada ya kuona gari la Polisi
-
Shuhuda mmoja alisema kuwa maaskari baada ya kuwakosa chuoni walienda uraiani kuwatafuta, alisema mtoto mmoja aliwaelekeza Polisi wanafunzi hao walipojificha
-
Shuhuda huyo alisema alisikia mlio wa bunduki na alipotoka alimkuta askari anabadilisha mavazi yake na kubakia na nguo za kiraia
-
Kwa upande wa mashuhuda wengine wamesema kuwa polisi huyo aliyemuua mwanafunzi anafahamika ni Afisa wa jeshi la polisi la kituo cha Nchiru.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK