AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Korea Kaskazini imekuwa ikiwatumia
vifaa Syria ambavyo vinaweza tumika katika kutengeneza silaha za
kemikali, ripoti ya chombo cha habari Marekani imesema kikinukuu ripoti
kutoka Umoja wa Mataifa.
Shutuma hizo zinakuja baada ya ripoti mpya ya utumiaji wa gesi ya chlorine na vikosi vya Syria, shutuma hizo zimekanushwa na serikali.
Korea Kaskazini ipo chini ya vikwazo vya kimataifa sababu ya programu yao ya nuklia.
Vifaa hivyo vinaripotiwa kupatikana kiwizi na kutumwa Syria na Korea Kaskazini vikiwemo vigae venye uwezo wa kuzuia joto na tindi kali mwingi na vipima joto. Vigae vinasemekana kutumika katika kujenga majengo ambapo silaha za kemikali zitatengenezwa.
Inasemekana wamtumiwa makumi ya mizigo ndani ya miaka kadha.
Gazeti hilo linasema, taasisi ya utafiti ya maswala ya sayansi ya Syria inasemekana kuwalipa Korea Kaskazini kupitia makumpuni bandia.
Serikali ya Syria imeripotiwa kuiambia Umoja wa Mataifa kuwa raia wa Korea Kaskazini waliopo Syria ni makocha na wanariadha tu.
Syira iliungana na mkutano wa silaha za kemikali na kukubali kuteketeza silaha hizo mwaka 2013 baada ya shambulio lililotumia gesi ya sarin na kuwaua mamia ya watu Ghouta.
Tangu mwaka huo, imeshutumiwa kwa kutumia silaha hizo marufuku mara kwa mara katika vita hiyo ya wenyewe kwa wenyewe.
Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.
Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA
Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK